Rais Kikwete atembelea kiwanda cha saruji kikubwa zaidi duniani cha Dangote, Nigeria
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete
ametumia siku nzima ya Ijumaa, Mei 9, 2014, kutembelea kiwanda kikubwa
zaidi cha saruji kuliko kingine chochote duniani cha Dangote Cement
Obajana Plant na kinachomilikiwa na tajiri mkubwa zaidi wa Afrika, Bwana
Aliko Dangote, ambaye pia anajenga kiwanda kikubwa cha saruji mjini
Mtwara.
Mbali
na Nigeria na Tanzania, Bwana Dangote ana viwanda ama anajenga viwanda
vya saruji ama na shughuli za saruji katika nchi 14 za Afrika ikiwamo
Ethiopia, Zambia, Mozambique, Kenya, Senegal na Sierra Leone, Afrika
Kusini, Congo (Brazzaville), Cameroun, Ghana, Liberia na Ivory Coast.
Mbali na shughuli za uzalishaji wa saruji, Bwana Dangote ambaye anakubaliwa kuwa tajiri mkubwa zaidi katika Afrika kwa thamani ya dola za Marekani bilioni 25 yeye na kampuni yake ya Dangote Group pia ina shughuli za uzalishaji wa sukari, uzalishaji wa chumvi, utengenezaji wa magunia, uzalishaji maji, uzalishaji wa vyakula vya aina mbali mbali, uzalishaji wa mafuta ya kupikia, utengenezaji wa nyanya.
Mbali na shughuli za uzalishaji wa saruji, Bwana Dangote ambaye anakubaliwa kuwa tajiri mkubwa zaidi katika Afrika kwa thamani ya dola za Marekani bilioni 25 yeye na kampuni yake ya Dangote Group pia ina shughuli za uzalishaji wa sukari, uzalishaji wa chumvi, utengenezaji wa magunia, uzalishaji maji, uzalishaji wa vyakula vya aina mbali mbali, uzalishaji wa mafuta ya kupikia, utengenezaji wa nyanya.