Header Ads

Matumizi Ya Kiswahili ZINDUKA yataka kitumike kwenye mijadala Afrika Mashariki




Jumuiko la makundi mbalimbali ya kijamii kutoka nchi za Afrika Mashariki kupitia umoja wao unaojulikana kama “ZINDUKA”,limekuja na mapendekezo ya kutaka matumizi rasmi ya lugha ya Kiswahili, katika mijadala na mikutano yote ya jumuiya ya Afrika mashariki.



Katika uwasilishwaji wa mapendekezo kutoka katika kusanyiko hilo la “ZINDUKA” lililokuwa likifanyika Jijini Arusha, ni kwamba Kiswahili hakijapewa uzito unaostahili ndani ya Afrika Mashariki.

Mmoja wa wasilishaji wa mapendekezo hayo Hezekiel Gikambi mhariri wa jarida la Swahilihub kutoka Kenya amesema katika jumuiya zote za afrika na hata ulaya hakuna hata moja miongoni mwazo ambayo ina lugha moja lakini Afrika mashariki ina Kishwahili ambacho hata hivyo hakitumiki ipasavyo

Masuala mengine yaliyozungumzwa katika kusanyiko hilo ni pamoja na kuzorota kwa hali ya usalama nchini Burundi,uimarishwaji wa huduma za kijamii na ukuzaji wa sekta za michezo,utalii na kilimo ndani ya jumuiya pamoja na mwito kwa viongozi kufuata katiba za nchi zao

TAFSIRI....“Mgeni yeyote anayetembele moja ya nchi za Afrika Mashariki aweze kufanya hivyo pasipo kuulizwa VISA tofauti bali kuwepo na VISA ya aina moja”alisema Willester Simiyu ambaye ni mshiriki wa zinduka

Mratibu wa “ZINDUKA” Amani Mhinda amesema mapendekezo yote yatapelekwa kwa Sekretariet na Bunge la jumuiya ya Afrika mashariki ili yaweze kufanyiwa kazi


Jumuiya ya Afrika Mashariki inaundwa na nchi za Tanzania,Kenya,Uganda,Rwanda na Burundi huku kukikadiriwa kuwepo na wakazi zaidi ya milioni 150 katika ukanda huu.
Powered by Blogger.