Header Ads

Serikali yashauriwa kutenga bajeti ya kununua vifaa tiba ili Kupunguza Vifo Vya Watoto



SERIKALI imepewa changamoto ya kutenga fedha katika bajeti yake na kununua vifaa tiba pamoja na dawa zitakazosaidia kupunguza au kuondoa kabisa vifo vya watoto wachanga hapa nchini ambapo ripoti mbalimbali zinaonyesha mwaka jana pekee imefikia watoto elfu kumi na tatu.


Changamoto hiyo imetolewa na Taasisi ya Doris Mollel Foundation muda mfupi baada ya kukabidhi vifaa vitakavyosaidia kuokoa maisha ya watoto wachanga hususani watoto njiti katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Iringa.

Ndani ya chumba cha joto, katika hosptali ya rufaa ya Mkoa wa Iringa, kila siku kinapokea watoto njiti wasiopungua sita ikiwemo watoto wenye matatizo ya uzito uliopitiliza na huhitaji matababu mazuri ili kuokoa uhai wao ikiwemo kuongezewa hewa ya oxygen kupitia machine ziitwazo Oxygen Concentrator ambayo ni moja ya vifaa vilivyotolewa na Taasisi hiyo

Mkuu wa Idara ya watoto katika hospitali hiyo,Dr.Florida Kigosi amesema uhitaji wa mashine hizo ni angalau mashine sita ambapo walizokuwa nao ni nne lakini zilizokuwa zinafanya kazi ni tatu tu na sasa baada ya kupata msaada watakuwa na mashine nne

Pamoja na mashine hiyo, vifaa vingine vilivyotolewa ni nguo mbalimbali,  mipira 500 ya kulishia watoto wa aina hiyo ambapo Wauguzi wa chumba hicho cha watoto njiti wameishukuru Taasisi hiyo huku Mkuu wa Mkoa wa Iringa,akikitaka kitengo cha Malaria katika hospitali hiyo kuwa na mipango endelevu itakayosaidia wajawazito kutojifungua watoto njiti kutokana na kuugua malaria

Ripoti ya mwaka juzi ya Shirika la kuhudumia Watoto Duniani UNICEF inasema kuwa mwaka juzi watoto 9000 walipoteza maisha kutokana na matatizo mbalimbali ikiwemo kuzaliwa njiti wakati Ripoti ya Shirika la Mama Yee, inasema mwaka jana idadi ya vifo vya watoto wa aina hiyo ilifikia watoto13,000.


Powered by Blogger.