KIJANA AUAWA NA WANANCHI KWA TUHUMA ZA WIZI WA TV NA SOLAR WILAYANI KAHAMA
Tukio hilo limetokea leo majira ya saa tatu asubuhi baada ya kudaiwa kuwa mtuhumiwa huyo alikutwa ndani kwenye nyumba ya jirani ambayo hata hivyo haijatajwa, ambapo alijifungia ndani kabla ya wananchi kuvunja mlango na kumtoa.
Imedaiwa kuwa Kijana huyo amewawa akituhumiwa kuhusika na wizi wa TV na Solar katika maeneo ya mtaa huo, na kwamba amekuwa akifanya uhalifu mara kwa mara lakini amekuwa akiendelea kuonekana mtaani hata baada ya kukamatwa na polisi.