Header Ads

Wauguzi Z’bar wahimizwa kufuata misingi ya taaluma




Katika kuhakikisha jamii inapatiwa huduma bora hususani za afya wanafunzi wa chuo cha sayansi ya afya Mbweni kilichopo visiwani Zanzibar   wametakiwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo ili   kuihudumia jamii  kwa kufuata misingi  ya taaluma  zao.


Hali hiyo itasaidia   kupunguza malalamiko kwa wagonjwa   ambao kwa kiasi   kikubwa   kada ya uuguzi ndiyo    inayolalamikiwa kutokana     na  baadhi ya wahudumu wa afya  kutoa lugha  chafu   pale wanapowahudumia wagonjwa.

Baadhi ya kazi  zilizoonyeshwa   na wanafunzi  wa chuo  hicho ikiwa  ni   mafunzo wanayofundishwa   ni  kwa jinsi gani  watatoa   huduma kwa wagonjwa   pale wanapofika katika vituo vya afya kutokana na ugonjwa husika , ikiwa ni maonyesho ya tano  ya  umoja wa wanafunzi wa  chuo hicho yanayofanyika  kila  mwaka chuoni hapo.

Licha ya kuonyesha kazi hizo Mkurugenzi wa  Utumishi na Rasilimali Watu  kutoka wizara  ya afya omary mwinyinkondo anasema  itakuwa vyema  basi yale waliyoyafanya  chuoni haapo yakataekelezwa  hata pale wanapopata nafasi yakuwahudumia wagonjwa , kwa kuwa imebainika kuwa  wafanyakazi  wengi  pale wanapopata mikataba  maadili  wanayaacha vyuoni na kushindwa  kutekeleza  sehemu za kazi na  kuondosha imani kwa wagonjwa.

Akizungumza   kwa niaba ya wanafunzi , rais  wa chuo hicho  sleiyoum abdallah ali anasema kuwa  licha ya kuonyesha kazi hizo bado wanakabiliwa na changamoto nyingi ya vitendea  kazi .

walimu wakisisistiza maadili hayo  kwa wanafunzi  basi malalamiko yatapungua  sehemu za kazi sanjari na  watumishi wenyewe  wakiwa tayari kufuata  missing hiyo ikiwa ni maoni ya  baadhi ya wanafunzi wa chuo hicho.

Sula la kufuata maadili katika utendaji kazi ni ya kila  kada  hivyo  ni  wajibu kutekeleza maadili hayo kivitendo ili   kuepuka  mawazo hasi  kwa wanajamii kuhusu  kada husika.



Powered by Blogger.