Header Ads

CWT Iringa yaunga mkono juhudi za Rais Magufuli kupambana na ubadhirifu



CHAMA cha walimu Tanzania CWT tawi la Iringa kimesema jitihada zinazofanywa na uongozi wa awamu ya tano ya rais Dr.John Pombe Magufuli  zinapaswa kuungwa mkono na watanzania wote wenye fikra pevu na nia njema ya maendeleo ya Taifa.


Zuio la posho kwa watumishi wa serikali, matumizi holela ya fedha za umma pamoja na kutafuta njia mbadala ya namna ya kusherekea siku ya Uhuru na maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani, ni miongoni mwa mambo yanayotajwa kuwa na tija  kwa jamii badala ya manufaa ya watu binafsi.
   
Kada ya Ualimu ni miongoni mwa taaluma ambazo zimekuwa zikilalamikia kukabiliwa na changamoto mbalimbali yakiwemo mazingira duni duni ya kazi.

Lakini kwa sasa tasnia hii ya Ualimu inaona uongozi wa awamu ya tano wa rais Dr. John Magufuli ni kama unawapa nuru ya mafanikio yenye kuchochea kasi ya utendajikazi.

Suala la kuondolewa kwa posho katika vikao mbalimbali vya watumishi wa Umma, ni miongoni mwa mambo yanayotajwa kuwa yatachangia kuleta usawa baina yao.

 Zawadi Mgongolwa ni mwenyekiti wa CWT Manispaa ya Iringa anasema njia sahihi ya kuyafikia maendeleo - ni watanzania kwa pamoja kuuunga mkono uongozi wa awamu ya tano wa rais Dr. John Magufuli kwa kufanyakazi kwa bidii.


Aidha uongozi huu wa CWT Manispaa ya Iringa unasema kitendo cha rais kutafuta mbadala wa matumizi ya fedha kwa ajili ya sherehe ni njia sahihi na yenye tija katika kujenga uchumi wa Taifa.
  
CWT Manispaa ya Iringa inasema hatua ya kuupongeza uongozi huo wa awamu ya tano, ni baada ya kuona dalili njema za utendaji wa kazi – ambao umekunjua nyuso za watanzania walio wengi hasa walimu, ambao kilio chao kikuu ni maisha duni pamoja na mazingira  yakazi yasiyo rafiki.



Powered by Blogger.