Header Ads

Mahakama kuu Zanzibar yakanusha taarifa ya Mwanahalisi



Mahakama kuu ya Zanzibar imekanusha vikali taarifa iliotolewa na Gazeti la mwanahalisi linalochapishwa kila wiki nchini iliodai kuwa Mahakama kuu Zanzibar inampango wa kuandaa mazingira ya kuwatumia wanasheria wakujitegemea kuweza kufunguwa kesi zinazohusu masuala ya uchaguzi kwa Makamishna wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar na wahusika wengine.


Imeelezwa taarifa hizo zinazodai mahakama inatumika  ni za uchochezi na kutaka kushusha hadhi ya mahakama.

Pamoja na mambo mengine wametowa siku saba kwa Gazeti hilo kuomba Radhi vinginevyo Mahakama itaangalia namna ya kufuata taratibu za kisheria dhidi ya gazeti hilo.

Akizungumza  na wanahabari  Ofisini kwake mahakama kuu Zanzibar Mrajisi wa mahakama kuu joge Kazi  anasema ameshangazwa na taarifa ya gazeti hilo ambalo amedai limeshidwa hata kufanya utafiti wa kufika ofisi za mahakama ili kujiridhisha na hali hiyo.

Aidha Joge Kazi anasema taratibu za kimahakama sio kutafuta kesi bali ni kupokea kesi kutoka kwa mkurugenzi wa mashtaka  na wala  sio mahakama kuu na kulitaka gazwti hilo kuacha kuandika taarifa za kichochezi hasa katika kipindi hiki cha mpito kwa Zanzibar.

Pamoja na mambo mengine Joge kazi anawataka waandishi wa habari kuzingatia maadili ya kazi zao waache kuchochea na kukubali kutumiwa kisiasa hali ambayo inaweza kusababisha uvunjifu wa amani nchini.


Powered by Blogger.