Header Ads

Watu wenye uwezo watakiwa kuisaidia Serikali Kupambana Na Umasikini



Watu wenye uwezo wa kifedha wameaswa kujitoa kuisaidia serikali katika kupambana na janga la umasikini nchini ikiwa pamoja na kuwainua kiuchumi baadhi ya wananchi wasiojiweza kimaisha.


Rai hiyo imetolewa katika hafla ya kuwatunuku shahada ya uzamivu baadhi ya watendaji wa serikali pamoja na Baadhi ya watu wanaofanya kazi kiroho iliyofanyika Jijini Mwanza.


Chuo cha Africa Graduate University, makao makuu yake  nchini Sierra Leone limejikita mkoani Mwanza Kutunuku vyeti Vya heshima shahada ya Udokta

Kufanya kazi kwa weledi kwa watumishi wa Serikali , kusaidia jamii katika masuala mbalimbali pamoja na kazi za kumtumikia Mungu ndio nguzo kuu kwa chuo hiki.

Ambapo wahitimu 10 wametunukiwa vyeti kutoka serikalini  pamoja na wachunguji ikiwa ni sehemu ya kuonesha Heshima na Uthamini  wa juhudi ya kuihudumia jamii.

Kutunukiwa kwa vyeti hivyo inaashiria tayari wanashahada ya udaktari katika kuwajibika vyema kwa nafasi zao

Awali katika hafla hivyo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo Shabaha yake ni umuhimu wa vyeti hivyo kutia moyo  watumishi na kuwajibika Ipasavyo.

Baadhi ya watunukiwa wanabainisha uhalali wa kutunukiwa vyeti na chuo hicho huku kilio chao kikibaki kwa tu wenye uwezo nao kujitoa kusaidia jamii katika masuala mbalimbali.

Hafra hiyo imehudhuriwa na viongozi Mbalimbali wa kidini na serikali


Powered by Blogger.