Header Ads

Zaidi watu 1,000 warejea kwenye tiba mkoani Sngida Kupunguza Makali Ya Vvu



ZAIDI ya watu elfu moja wanaoishi na Virusi vya ugonjwa wa UKIMWI katika Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida, wamerejea kwenye tiba baada ya kuacha kabisa kuhudhuria Kliniki maalum za kuwahudumia miaka mitatu iliyopita kutokana na sababu mbalimbali.


Sababu za kuacha dawa za kufubaza Virus zinatajwa kuwa ni Kikombe cha Babu wa Loliondo, unyanyapaa na wengine kudhani kuwa wamepona hivyo kuendelea kudhofika hadi walipofikiwa na mpango wa huduma majumbani unaoendesha na Shirika la SEMA Singida na kurejeshwa kwenye tiba.

Siku chache baada ya Serikali kusitisha maadhimisho ya siku ya UKIMWI Dunia, yaliyopangwa kufanyika Kitaifa mkoani Singida mwaka huu, Shirika la SEMA-Singida linalojishughulisha na mapambano dhidi ya ugonjwa huo, limejitokeza kuelezea mafanikio ya mradi wake wa huduma majumbani.

Zipo sababu zinazotajwa kuchangia baadhi ya watu kuacha kutumia dawa za kufubaza virusi vya UKIWMI ikiwemo garama za kununulia dawa.

Baadhi ya watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI wameleza maisha yao ya awali na jinsi mpango huo wa huduma majumbani ulivyosaidia kuboresha maisha na kupunguza unyanyapaa katika jamii.

Chini ya mpango huo unaofadhiliwa na Mradi wa Tunajali, tangu mwaka 2012 zaidi ya shilingi milioni 300 zimetumika kutoa huduma majumbani kwa watu 1,705 wanaoishi na virusi vya UKIMWI Wilayani Iramba.



Powered by Blogger.