Header Ads

Wachimbaji wadogo watano wafariki Geita


Wachimbaji wadogo watano wamefariki dunia baada ya kufukiwa na vifusi katika maeneo ya Mgusu na Nyanza mkoani Geita.


Matukio hayo yametokea kwa nyakati tofauti ambapo wachimbaji kumi waliingia eneo la Nyanza majira ya saa tisa novemba 28 na wakiwa katika harakati za uchimbaji wakaangukiwa na kifusi huku usiku wa novemba 29 tukio hilo limetokea mgusu na kusababisha wachimbaji hao kufariki.

Maeneo ya Nyanza na Mgusu wanayoingia wachimbaji wadogo kwa ajili ya kujitafutia dhahabu yako chini ya Mgodi wa Dhahabu wa Geita.

Wachimbaji hao wanasema tukio la kufukiwa kwa wenzao wa mgusu walipata taarifa usiku wa saa sita ndipo walipotoa taarifa kwa wenzao na kuanza zoezi la uokoaji ambapo walifanikiwa kutoa miili.

Waliofariki ni Emanuel Emanuel,Luca Deus,Maliatabu Budonyanga,Clement Richard na Baraka Katunzi ambaye bado walikuwa wanafanya jitihada za kumtafuta.

Zoezi la uokoaji limefanyika kikamilifu asubuhi na kufanikiwa kuoa maiti nne huku mmoja akiwa bado anatafutwa katika kifusi hicho.

Wachimbaji hawa ambao wamekuwa wakihatarisha maisha yao kuingia maeneo ambayo ni hatarishi ambapo novemba 28 eneo la nyanza majira ya mchana walifukiwa wachimbaji kumi lakini kwa juhudi za mgodi wakafanikiwa kutolewa wakiwa hai.

Vijana hawa wamedai kujihatarishia maisha kutokana na kukosa ajira na njia pekee wanayoitegemea ni uchimbaji kwahiyo huwa wanangalia eneo rahisi linalopatikana dhahabu na kwenda kuanza kuchimba.
  
Wachimbaji hawa wadogo hawako rasmi jambo ambalo limekuwa gumu kuwawezesha kwa pamoja na kuwataka wafuate taratibu kwani serikali inafanya jitihada za maeneo kwa ajili ya wachimbaji.


Powered by Blogger.