Header Ads

Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Profesa Sospeter Muhongo akutana na Ujumbe kutoka Benki ya Dunia Kujadiliana Kuhusu Masuala ya Gesi Nchini

Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akiongoza kikao kati yake na Ujumbe  kutoka Benki ya Dunia pamoja na Watendaji wa Wizara. Kikao hicho kimejadiliana kuhusu suala zima la Gesi nchini na hatua mbalimbali zilizofikiwa hadi sasa.

Waziri wa Nishati na Madini Mhe.Profesa Sospeter Muhongo amekutana na Ujumbe kutoka Benki ya Dunia kuzungumzia Masuala ya Gasi nchini. Miongoni mwa Masuala yaliyojadiliwa katika kikao hicho ni kuhusu hatua mbalimbali ambazo zimefikiwa hadi sasa na Serikali kuhusu Sekta hiyo. Aidha, kikao hicho pia kimewashirikisha Watendaji kutoka Wizara hiyo wanaosimamia masuala ya Gesi Asilia na Nishati.
 Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akiongoza kikao kati yake na Ujumbe  kutoka Benki ya Dunia pamoja na Watendaji wa Wizara. Kikao hicho kimejadiliana kuhusu suala zima la Gesi nchini na hatua mbalimbali zilizofikiwa hadi sasa.
 Kamishna Msaidizi anayesimamia Masuala ya Gesi Asilia Engineer. Bw. Nobert Kahyoza akifafanua jambo wakati wa kikao hicho.
 Kamishna Msaidizi anayesimamia Maendeleo ya Nishati Bw. James Andilile  akisisitiza jambo wakati wa kikao hicho baina ya Wizara na Ujumbe toka benki ya Dunia.
Powered by Blogger.