Header Ads

Kamati ya ardhi,maliasili na mazingira yatembelea hifadhi ya taifa ya Mlima Kilimanjaro

Mkurugenzi mkuu wa shirika la hifadhi za jamii Tanzania,TANAPA,Alan Kijazi akizungumza jambo wakati kamati ya Bunge ya ardhi,maliasili na mazingira ilipotembelea hifadhi ya taifa ya Mlima Kilimanjaro.
Baadhi ya wajumbe wa kamati ya Ardhi,maliasili na mazingira wakifuatilia maelezo ya mkurugenzi mkuu wa TANAPA(hayupo picani).
Naibu waziri wa maliasili na Utalii,Mahamud Mgimwa akizungumza mbele ya kamati ya Ardhi ,maliasili na mazingira ilipotembelea hifadhi ya taifa ya mlima Kilimanjaro.
Mhifadhi mkuu wa hifadhi ya taifa ya mlima Kilimanjaro ,Erasimus Lufunguro akitoa maelezo kuhusu nusu maili katika mlima Kilimanjaro kwa kamati ya Ardhi ,maliasili na mazingira ilipotembelea hifadhi ya taifa ya mlima Kilimanjaro.
Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Ardhi,maliasili na Mazingira,Mh James Lembeli akizungumza wakati kamati hiyo ilipokutana na maofisa wa TANAPA na KINAPA katika ofisi za Hifadhi ya mlima Kilimanjaro.
Mjumbe wa kamati ya Ardhi ,maliasili na Mazingira,Suzan Kiwanga akichangia jambo wakati kamati hiyo ilipotembelea hifadhi ya taifa ya mlima Kilimanjaro.
Eneo la nusu maili katika mlima kilimanjaro ambalo zamani lilitumiwa na wakazi walioko jirani na eneo hilo kwa shughuli za kukata Nyasi na badala yake walikata miti kabla ya kurejeshwa katika hifadhi ya taifa ya KINAPA kwa ajili ya usimamizi ambapo hifadhi sasa limeanza kurejea katika hali yake baada ya miti kuoteshwa.
Mjumbe wa kamati ya Ardhi,maliasili na mazingira Lekule Laizer akizungumza jambo mbele ya wajumbe wenzake na naibu waziri wa maliasili na utalii,Mahamud Mgimwa.
Wajumbe wa kamati wakiwa katika eneo la Nusu maili katika mlima Kilimanjaro.
Mkurugenzi mkuu TANAPA ,Alan Kijazi akiwa na mhifadhi mkuu wa KINAPA Erasimus Rufunguro wakisilikiza kwa makini jambo kutoka kwa mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi,maliasili na Mazingira,Mh James Lembeli(hayupo pichani).
Mwenyekiti wa kamati ya Ardhi ,maliasili na mazingira,James Lembeli akizungumza jambo wakati kamati hiyo ilipotembelea hifadhi ya mlima Kilimanjaro.
Mwenyekiti wa kamati ya Ardhi maliasili na mazingira,James Lembeli akimsadia kumbebesha mzigo wa kuni mmoja wa wakazi wanaoishi jirani na mlima Kilimanjaro aliyekuwa akiokota kuni katika eneo la nusu maili. Na Dixon Busagaga wa globu ya jamii Moshi.
Powered by Blogger.