Header Ads

SALAAM KWA YANGA MBELE YA MKWASA JUKWAANI!!



SALAAM KWA YANGA MBELE YA MKWASA JUKWAANI!!
MOHAMED_ABOU_TRIKAMABINGWA wa AFRIKA, Al-Ahly ya Misri, wametwaa Kombe la CAF SUPER CUP baada ya kuichapa Klabu ya Tunisia CS Sfaxien Bao 3-2 Uwanja wa Kimataifa wa Cairo Jijini Cairo, Nchini Misri.
CAF SUPER CUP hushindaniwa kila Mwaka na Bingwa wa CAF CHAMPIONZ LIGI na Timu inayotwaa CAF Kombe la Shirikisho na safari hii Al Ahly walicheza kama Bingwa wa CHAMPIONZ LIGI na CS Sfaxien ndio waliotwaa Kombe la Shirikisho Mwaka Jana.
Wakishangiliwa na Mashabiki wao 30,000, Al Ahly walitangulia kufunga Bao kupitia Straika Mohamed 'Gedo' Nagy ambalo lilidumu hadi Haftaimu.
Kipindi cha Pili, Amr Gamal aliipa Al Ahly Bao la Pili na Fakhreddine Ben Youssef kuifungia CS Sfaxien Bao lao la kwanza lakini Amr Gamal tena akapiga Bao la 3 kwa Al Ahly.
Nahodha wa CS Sfaxien, Ali Maaloul, alileta mshikemshike kwenye Mechi hii baada ya kufunga Penati na kufanya Gemu iwe 3-2.
Lakini Al Ahly walisimama imara na kulinda Bao zao na kutwaa SUPER CUP hii ikiwa ni mara ya 6 na ni rekodi na kuwaacha CS Sfaxien wakishikilia rekodi ya kulikosa Kombe hili mara tatu.
Ushindi huu ni ahueni kubwa kwa Kocha wa Al Ahly, Mohamed Youssef, ambae Timu yake imechapwa mara 3 kwenye Ligi yao na Timu dhaifu.
Miongoni mwa Watazamaji wa Mechi hii ni Kocha Msaidizi wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa, ambae alipelekwa rasmi Jijini Cairo kuichunguza Al Ahly ambayo watakutana nayo kwenye Mechi ya Raundi ya Kwanza ya CAF CHAMPIONZ hapo Machi Mosi Jijini Dar es Salaam.
Powered by Blogger.