Header Ads

" Kufungwa tumefungwa, lakini msosi wa Dar es Salaam mtamu...!"

Jioni hii kwenye mgahawa niupendao Dar walitinga washabiki wa Al Ahly waliosafiri toka Cairo kuja kuishangilia timu yao. Wananiambia wamekuja Dar kuishangilia timu yao itoke sare au ifungwe moja tu! Wanasema wana uhakika wa kuifunga Yanga Cairo, wasichokijua ni idadi ya magoli...!
Mtazamo wangu; Yanga wamecheza vizuri. Wamewalazimisha Al Ahly kwao kufanya mawili magumu; kuzuia wasifungwe na lazima wafunge. Yanga hawatakiwi kabisa kujihami. Wacheze kama vile wao ndio wenye kuhitaji goli moja. Ni ushauri tu bila kujali kuwa anayeutoa ni Simba damu...
Maggid,
Dar.(P.T)
Powered by Blogger.