Header Ads

JIFANU CREATION GROUP IMEITAKA SERIKALI KUIPA KIPAUMBELE SANAA HAPA NCHINI.





Serikali pamoja na mashirika binafsi yametakiwa kuvipa vipaumbele vikundi mbalimbali vya sanaa hapa nchini kwa kuvisaidia kifedha kwakuwa vimekuwa ni nyenzo muhimu yakufikisha ujumbe na  kuielimisha jamii.
Hayo yamesemwa na viongozi wa Taasisi ya JIFANU ARTS CREATION katika maeneo ya Unga LTD jiji Arusha walipoongea na Habarijamii wakieleza namna wanavyofanya shughuli zao katika jamii kwakujitolea na kufanikiwa kubadili mitazamo ya jamii.
Mkurugenzi mkuu wa Tasisi hiyo Bwana  Eliya Masavel amesema sanaa imekuwa na umuhimu mkubwa sana katika jamii kwa kuwa na mtazamo wenye kuleta tija ndani na nje ya ngazi za familia na tamaduni mbalimbali.
Amesema licha ya kufanya kazi hizo zikiwemo uhamasishaji wa Elimu,Utunzaji wa mazingira,Afya pamoja na mambo mengine lakini serikali pamoja na mashirika binafsi hazina ukaribu na vikundi hivyo  jambo ambalo linakwamisha malengo yao kuweza kutimia.
Kwa upande wa viongozi wengine wa Taasisi hiyo Bw Genesis Roulen na Bw Ally Juma wamesema kuwa wamefanikiwa kupunguza tatizo la utapia mlo lililokuwa likiwakabili jamii nyingi,kupinga unanyasaji kwa watoto pamoja na mambo mengine ikiwa ni moja ya malengo yao.
Powered by Blogger.