Header Ads

NINI WAMESEMA BAADA MECHI: MOURINHO v MOYES!

>>MOURINHO: “WALIANZA VYEMA KUPITA SISI….TUNA MUUAJI KWENYE BOKSI!”
>>MOYES: “HATUKUSTAHILI BAO 2-0 NYUMA HAFTAIMU..YA VIDIC SI NYEKUNDU!
MOYES_v_MOURINHOMARA baada ya Chelsea kuichapa Manchester United Bao 3-1 Uwanjani Stamford Bridge kwa Hetitriki ya Samuel Eto’o, Mameneja wa Klabu hizo mbili walihojiwa na kujibu ifuatavyo:
-JOSE MOURINHO:
"Nadhani huu ni ushindi mkubwa na tumestahili, ndio. Jinsi nilivyokuwa nikichambua Gemu ilikuwa ngumu kwao kuwa nyuma 2-0. Walianza vyema kupita sisi, walikuwa juu. Kipindi cha Pili kilikuwa tofauti. Kwa Dakika 25-30 tulitawala lakini wakaja juu. Nadhani hii gemu iko tofauti na nyingine. Kawaida tunatawala hatufungi lakini leo shuti la kwanza tumefunga. Goli la pili lilikuwa ni la Muuaji kwenye boksi ambae namjua Miaka mingi na inaonekana kama Samuel Eto'o anarudi tena.”
-Kuhusu Ubingwa kwa Man United, Mourinho alisema: “Ni ngumu, wako Pinti 14 nyuma ya Arsenal, 13 nyuma ya Man City na 12 nyuma yetu. Labda Timu moja itasambaratika lakini si zote Tatu, ni ngumu, kwao nadhani sasa ni kupigania kumaliza 4 bora. Watafanya hivyo kwani ni Klabu yenye fahari na utamaduni na watapigana na kushinda dhidi ya wapinzani wengine kwa vile hatuchezi nao tena.”
-DAVID MOYES:
"Hatukustahili kuwa nyuma Bao 2-0 Haftaimu. Tulikuwa na bahati mbaya kwa Bao la Kwanza lakini yale mawili mengine tujilaumu wenyewe. Hatukujihami vizuri na hatukupata nafasi kama Chelsea kufunga. Tulicheza vizuri baadhi ya gemu. Tulicheza vizuri mwanzoni, tulishindwa tu umaliziaji. Hatukufunga kwenye boksi lao, tulishindwa kujihami boksi letu. Nadhani tulicheza vizuri katikati, hatukufanya vyema sehemu muhimu. Hatukati tamaa, tutaendelea na kuboresha kila sehemu, mie na Klabu tutafanya hilo.”
-Kuhusu Kadi Nyekundu kwa Vidic na Kadi ya Njano kwa Rafael, Moyes  alisema:
"Sikuiona ya Rafa lakini niliona ya Vidic. Ya Vidic si Nyekundu ni Njano. Kama ya Rafa ni mbaya basi nitakuwa mkweli na kujitokeza kusema hilo.”
Powered by Blogger.