Header Ads

TAIFA STARS KUIKABILI NAMIBIA HUKO WINDHOEK!

>>30 TWIGA STARS WAITWA KUIVAA ZAMBIA
>>RAMBIRAMBI MSIBA WA KANALI MMARI
>>MAOFISA TFF KUKAGUA VIWANJA 19 VYA VPL, FDL
>>RAIS MALINZI KUFUNGA SEMINA YA WAAMUZI LEO
TAIFA_STARS-FRAMEDSOMA ZAIDI:
Release No. 005
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Januari 14, 2014
30 TWIGA STARS WAITWA KUIVAA ZAMBIA
Kocha Mkuu wa Twiga Stars, Rogasian Kaijage ametaja kikosi cha wachezaji 30 wanaoingia kambini kesho (Januari 15 mwaka huu) jijini Dar es Salaam kujiandaa kwa mechi dhidi ya Zambia mwezi ujao.
Mechi hiyo ya kwanza ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Wanawake (AWC) zitakazofanyika baadaye mwaka huu jijini Windhoek, Namibia itafanyika jijini Lusaka.
Wachezaji walioitwa kwenye kikosi hicho ni Amina Ally (Lord Baden Sekondari), Amisa Athuman (Marsh Academy), Anastazia Anthony (Lord Baden Sekondari), Asha Rashid (Mburahati Queens), Aziza Mwadini (Zanzibar) na Belina Julius (Lord Baden Sekondari).
Donisia Daniel (Lord Baden Sekondari), Esther Chabruma (Sayari Queens), Evelyn Sekikubo (Kwimba Chuoni), Fatuma Bushiri (Simba Queens), Fatuma Hassan (Mburahati Queens), Fatuma Issa (Evergreen) na Fatuma Mustapha (Sayari Queens).
Fatuma Omari (Sayari Queens), Happiness Hezron (Copa Coca-Cola Ilala), Maimuna Hamisi (U20 Tanzanite), Maimuna Said (JKT), Mwajuma Abdallah (Real Tanzanite), Mwapewa Mtumwa (Sayari Queens), Najiat Abbas (Makongo Sekondari) na Neema Paul (U20 Tanzanite).
Pulkeria Charaji (Sayari Queens), Semeni Abeid (Real Tanzanite), Shelder Boniface (Makongo Sekondari), Sophia Mwasikili (Sayari Queens), Theresa Yona (TSC Academy), Vumilia Maarifa (Evergreen) na Zena Khamis (Mburahati Queens).
RAMBIRAMBI MSIBA WA KANALI MMARI
Shrikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha mwanzilishi wa wa timu ya Oljoro JKT, Kanali Mmari kilichotokea jana (Januari 13 mwaka huu) jijini Dar es Salaam.
Kanali Mmari ambaye aliasisi timu hiyo na kuifikisha hadi kwenye Ligi Kuu ya Vodacom amefia Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ambapo alikuwa amelazwa baada ya kupata ajali ya gari Chalinze mkoani Pwani, Januari Mosi mwaka huu.
Msiba huu ni mkubwa kwa jamii ya mpira wa miguu kwani mbali kuasisi timu ya Oljoro JKT alikuwa mhamasishaji mkubwa wa mchezo huo mkoani Arusha, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.
TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Kanali Mmari, klabu ya Oljoro JKT, Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Arusha (ARFA) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
Bwana alitoa, Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe. Amina
MAOFISA TFF KUKAGUA VIWANJA 19 VYA VPL, FDL
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeteua maofisa wanaoanza leo (Januari 14 mwaka huu) kukagua viwanja 19 vitakavyotumika kwa mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL).
Ukaguzi huo pia unahusisha viwanja ambavyo Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) ilizuia mechi za VPL na FDL kuchezwa mpaka hapo vitakapokuwa vimefanyiwa marekebisho ili kukidhi sifa za kutumiwa kwa mechi hizo.
Viwanja vinavyokaguliwa ni Ali Hassan Mwinyi (Tabora), CCM Kirumba (Mwanza), Jamhuri (Dodoma), Jamhuri (Morogoro), Kaitaba (Bukoba), Kambarage (Shinyanga), Kumbukumbu ya Karume (Musoma) na Kumbukumbu ya Samora (Iringa).
Kumbukumbu ya Sokoine (Mbeya), Lake Tanganyika (Kigoma), Mabatini (Pwani), Majimaji (Songea), Mbinga (Mbinga), Mkwakwani (Tanga), Mwadui (Shinyanga), Wambi (Mufindi, Iringa), Sheikh Kaluta Amri Abeid (Arusha), Umoja (Mtwara) na Vwawa (Mbozi).
Vyama vya mpira wa miguu vya mikoa husika na mameneja wa viwanja husika wanatakiwa kuwapa ushirikiano wakaguzi hao kutoka TFF.
RAIS MALINZI KUFUNGA SEMINA YA WAAMUZI LEO
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi atakuwa mgeni rasmi katika ufungaji wa semina ya waamuzi na makamisha leo (Januari 4 mwaka huu) saa 4 asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Waamuzi zaidi ya 100 na makamishna 50 wameshiriki katika semina hiyo. Makamishna hao ni baadhi ya wale wanaosimamia mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) wakati waamuzi ni wale wa daraja la kwanza (class one) ambao ndiyo wanaochezesha mechi za VPL na FDL.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatarajia kuandaa semina nyingine baadaye mwaka huu kwa makamishna wapya wanaotaka kusimamia mechi za VPL na zile za FDL.
Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari na Mawasiliano
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
+++++++++++++++++++++++++++++++++
Release No. 006
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Januari 14, 2014
TAIFA STARS KUIKABILI NAMIBIA FIFA DATE
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) itacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Namibia (Brave Warriors) ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya michuano ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika (AFCON) zitakazochezwa mwakani nchini Morocco.
Stars na Brave Warriors zitacheza mechi hiyo Machi 5 mwaka huu jijini Windhoek, Namibia. Mechi hiyo ipo katika kalenda ya mechi za kirafiki za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).
Makubaliano ya kucheza mechi hiyo yamefikiwa kutokana na mazungumzo kati ya Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi na Rais wa Chama cha Mpira wa Miguu Namibia (NFA), John Muinjo.
Benchi la Ufundi la Brave Warriors linaongozwa na kocha mzawa Ricardo Mannetti, na mechi hiyo itachezwa ama Uwanja wa Sam Nujoma au Uwanja wa Uhuru jijini Windhoek.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager inafundishwa na kocha Kim Poulsen kutoka Denmark na inatarajia kuanza kucheza mechi za mchujo za AFCON Septemba mwaka huu.
Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari na Mawasiliano
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Powered by Blogger.