Header Ads

BIGI MECHI LIVERPOOL v CHELSEA, MVUTO MAN UNITED v NORWICH..NI CLASS OF ‘92!


>JE MOURINHO KUPANGA KIKOSI 'DHAIFU' ANFIELD JUMAPILI??
LIGI KUU ENGLAND inaelekea patamu wakati Liverpool wakikaribia kutwaa Ubingwa wao waBPL2013LOGOkwanza tangu 1990 lakini kikwazo ni Bigi Mechi ya Jumapili huko Anfield ambako Jose Mourinho atatua na Chelsea yake wakiwa na matumaini finyu ya Ubingwa huku macho ya Wadau, hasa wa Manchester United, wakielekeza Old Trafford ambako Jumamosi wataikabili Norwich City wakiwa na Meneja mpya, Ryan Giggs, akiwa na Wataalam wenzake alioanza nao tangu Utotoni, ‘THE CLASS OF ‘92’, kina Phil Neville, Nicky Butt na Paul Scholes.
PATA DONDOO FUPI ZA MECHI ZA WIKIENDI:
+++++++++++++++++++++++
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA:
[Saa za Bongo]
Jumamosi 26 Aprili 2014
1445 Southampton v Everton
1700 Fulham v Hull
1700 Stoke v Tottenham
1700 Swansea v Aston Villa
1700 West Brom v West Ham
1930 Man United v Norwich
Jumapili 27 Aprili 2014
1400 Sunderland v Cardiff
1605 Liverpool v Chelsea
1810 Crystal Palace v Man City
+++++++++++++++++++++++
SOUTHAMPTON v EVERTON
-St Mary’s
Kikosi cha Roberto Martinez, kinachowania kumaliza 4 Bora, kinaelekea Ugenini huko kwa Mtakatifu Maria baada ya Bosi huyo wa Everton kumteketeza Bosi wa zamani wa Everton, David Moyes kwa kumchapa 2-0 huko Goodison Park na hiyo kuwa Mechi ya mwisho ya Moyes kama Meneja wa Manchester United.
Wakati Everton wana ushindi wa Mechi 3 mfululizo za Ugenini, Sourhampton wao hajwashinda katika Mechi zao 3 zilizopita.
FULHAM v HULL CITY
-Craven Cottage
Bosi wa Fulham, Felix Magath, amesisitiza Timu yake haitoshuka Daraja ikiwa itashinda Mechi zake 2 za Nyumbani zilizobaki na hii ni mojawapo.
Hull City wapo Wembley, kwenye Fainali ya FA CUP dhidi ya Arsenal, lakini kwenye Ligi wako kipindi kigumu baada kufungwa Mechi 4 kati ya 6 zilizopita za Ugenini.
STOKE CITY v TOTTENHAM HOTSPUR
-Britannia Stadium
Stoke City wapo kwenye wimbi zuri ambalo wamefungwa Mechi 1 tu katika 8 zilizopita lakini Tottenham, chini ya Meneja Tim Sherwood, hawatabiriki.
SWANSEA CITY v ASTON VILLA
-Liberty Stadium
Wikiendi iliyopita, Swansea waliifunga Newcastle Ugenini na Straika wao, Wilfried Bony, kufunga Bao zote mbili huko St James’ Park lakini Bony hajafunga Bao Uwanjani kwao Liberty Stadium tangu Februari.
Meneja wa Aston Villa, Paul Lambert, anaamini ushindi kwenye Mechi 1 kati ya 4 zilizobaki utawahakikishia kubaki Ligi Kuu England.
WEST BROMWICH ALBION v WEST HAM UNITED
-The Hawthorns
West Brom wako Pointi 3 juu ya ya zile Timu 3 za Mkiani ambazo hushushwa Daraja mwishoni mwa Msimu na ushindi dhidi ya West Ham, ambao wamefungwa Mechi 3 mfululizo, utawasogeza kwenye usalama hasa ukizingatia Mechi zao 2 zijazo ni ngumu ambazo ni dhidi ya Arsenal, inayowania 4 Bora, na Sunderland wanaopigania uhai wao.
MANCHESTER UNITED v NORWICH CITY
-Old Trafford
CLASS_OF_92Hii ni Mechi ya kwanza kwa Meneja mpya, Ryan Giggs, ambae kwenye Benchi lake atakuwa nao Wachezaji wenzake wa zamani alioanza nao kuchezea Man United tangu wakiwa na Miaka 12, kina Paul Scholes, Nicky Butt na Phil Neville.
Hii ni Mechi yenye mvuto sana, hasa kwa Wadau wa Man United, lakini ni Mechi ya ‘kufa kupona’ kwa Norwich City ambao wako Pointi 2 tu juu ya zile Timu 3 za Mkiani ambazo hushushwa Daraja mwishoni mwa Msimu.
JUMAPILI Aprili 27
LIVERPOOL v CHELSEA
-Anfield
Hii ni BIGI MECHI.
Lakini baada ya Chelsea kufungwa 2-1 na Sunderland Wikiendi iliyopita na kuondoa matumaini yao kutwaa Ubingwa na kufuatia wao kupata Sare ya 0-0 Ugenini na Atletico Madrid kwenye Mechi ya Kwanza ya UEFA CHAMPIONZ LIGI Juzi Jumanne, mkazo kwa Chelsea ni Ulaya na si England tena hasa kwa kuwa wanarudiana na Atletico Jumatano ijayo huko Stamford Bridge.ANFIELD_1
Hali hii imemfanya Jose Mourinho aombe ridhaa ya Uongozi wa Juu Chelsea kuchezesha Kikosi hafifu dhidi ya Liverpool ili kuwalinda Mastaa wao kwa Marudiano na Atletico Madrid na hasa kuwachezesha Wachezaji ambao Jumatano hawatacheza Mechi hiyo ya Ulaya.
Miongoni mwa hao ni Frank Lampard na John Mikel Obi ambao hawezi kucheza na Atletico baada ya kuzoa Kadi za Njano na hivyo kufungiwa kutocheza Mechi hiyo.
Pia, Chelsea haiwezi kuwatumia Nemanja Matic na Mohamed Salah kwenye Mechi na Atletico kwa vile hawaruhusiwi kucheza na UEFA.
Hivyo, Mourinho yuko huru kuwachezesha Lampard, Obi, Matic na Salah kwenye Mechi na Liverpool bila kuathiri mipango yake ya Gemu na Atletico.
Hata hivyo, Mourinho hawezi kumtumia Ramires ambae amefungiwa Mechi 4 za Ligi baada kukiri kosa la kumpiga Larsson wa Sunderland Wiki iliyopita tukio ambalo Refa Mike Dean hakuliona na Leo hii FA kumpata na hatia.
Liverpool, chini ya Brendan Rodgers ambae alikuwa Kocha wa Vijana na Timu ya Rizevu ya Chelsea wakati Mourinho ni Meneja wa Chelsea katika Kipindi chake cha kwanza kati ya 2004 na 2009, wanahitaji hata Sare kwenye Mechi hii na Liverpool ili wawe mstarini kutwaa Ubingwa lakini hadi sasa wameshashinda Mechi 11 mfululizo za Ligi.
Mourinho, ambae tayari ameshawananga Liverpool kwa kuwaita ‘Wafalme wa Penati’, huenda asikubali kufungwa na Liverpool na kushusha Kikosi thabiti.
SUNDERLAND v CARDIFF CITY
-Stadium of Light
Sunderlana, baada ya kuichapa Chelsea na kutoka Sare na Man City katika Mechi zao mbili zilizopita, sasa wanakutana na Klabu kama wao, Cardiff City, ambao wanasaka ushindi kwa Udi na Uvumba ili wabaki Ligi Kuu England.
Sunderland wako mkiani na juu yao ni Fulham na kufuatia Cardiff City wenye Pointi 1 zaidi ya Sunderland ambao wana Mechi 1 mkononi.
Hii ni Fainali kwa Timu zote mbili.
MAN_CITY-VICHWA_CHINI_BAADA_KICHAPOCRYSTAL PALACE v MANCHESTER CITY
-Selhurst Park
Wakati Mechi hii inaanza, Man City watakuwa tayari wanajijua wamesimama wapi baada ya Liverpool na Chelsea kumaliza kucheza.
Palace wanatinga kwenye Mechi hii wakiwa kwenye wimbi kubwa la ushindi wa Mechi 5 mfululizo na City wataingia wakiwakosa Wachezaji muhimu akiwemo Majeruhi Yaya Toure huku David Silva na Sergio Aguero wakiwa na maamuivu naARSENE_WENGER-13hamna uhakika kama watacheza.
ARSENAL v NEWCASTLE UNITED
-Emirates Stadium
Aaron Ramsey amerudi dimbani baada kupona na Lukas Podolski amepiga Bao 5 katika Mechi 5 zilizopita na Arsenal wamerudi tena kwenye Reli wakiwania 4 Bora.
Newcastle wao wametandikwa Mechi 5 mfululizo lakini safari hii Meneja wao, Alan Pardew, atakuwepo Benchi baada kumaliza Mechi 5 za Kifungo chake.
LIGI KUU ENGLAND:
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
Liverpool
35
25
5
5
96
44
52
80
2
Chelsea
35
23
6
6
67
26
41
75
3
Man City
34
23
5
6
91
35
56
74
4
Arsenal
35
21
7
7
62
41
21
70
5
Everton
35
20
9
6
57
34
23
69
6
Tottenham
35
19
6
10
51
49
2
63
7
Man United
34
17
6
11
56
40
16
57
8
Southampton
35
13
10
12
50
45
5
49
9
Newcastle
35
14
4
17
39
54
-15
46
10
Stoke
35
11
11
13
39
49
-10
44
11
Crystal Palace
35
13
4
18
28
41
-13
43
12
West Ham
35
10
7
18
38
48
-10
37
13
Swansea
35
9
9
17
47
51
-4
36
14
Hull
34
10
6
18
34
43
-9
36
15
Aston Villa
34
9
8
17
35
49
-14
35
16
West Brom
34
6
15
13
41
54
-13
33
17
Norwich
35
8
8
19
28
56
-28
32
18
Cardiff
35
7
9
19
31
65
-34
30
19
Fulham
35
9
3
23
35
77
-42
30
20
Sunderland
34
7
8
19
33
57
-24
29
+++++++++++++++++++++++++++++
RATIBA MECHI ZIJAZO:
[Saa za Bongo]
Jumatatu 28 Aprili 2014
2200 Arsenal v Newcastle
Jumamosi 3 Mei 2014
1445 West Ham v Tottenham
1700 Aston Villa v Hull
1700 Man Utd v Sunderland
1700 Newcastle v Cardiff
1700 Stoke v Fulham
1700 Swansea v Southampton
1930 Everton v Man City
Jumapili 4 Mei 2014
1530 Arsenal v West Brom
1800 Chelsea v Norwich
Jumatatu 5 Mei 2014
2200 Crystal Palace v Liverpool
Jumanne 6 Mei 2014
2145 Man Utd v Hull
Jumatano 7 Mei 2014
2145 Man City v Aston Villa
2145 Sunderland v West Brom
Jumapili 11 Mei 2014
[Mechi zote Saa 1700]
Cardiff v Chelsea
Fulham v Crystal Palace
Hull v Everton
Liverpool v Newcastle
Man City v West Ham
Norwich v Arsenal
Southampton v Man Utd
Sunderland v Swansea
Tottenham v Aston Villa
West Brom v Stoke
Powered by Blogger.