UTABIRI WA VIFO 20 KWA WASANII WA BONGO MOVIE WATAOKUFA MWEZI HUU ULIOTOLEWA NA NABII BANDERA WAWATISHA WASANII AKIWEMO LULU.
HUKU makovu ya maumivu ya kuondokewa mfululizo na mastaa wanne wa filamu za Kibongo katika kipindi cha mwezi mmoja yakiwa hayajapona nabii naye ameibuka na kuweka wazi utabiri wake mzito kuhusu wasanii nchini hivyo kuwa sanjari na Maalim Hassan Yahya Hussein.
Kabla ya kifo cha Mzee Small, mtabiri maarufu nchini, Maalim Hassan ambaye ni mrithi wa baba yake marehemu Sheikh Hussein Yahya alitabiri kutokea vifo zaidi hadi Aprili mwakani.
Akizungumza bila hofu na gazeti hili juzu, Nabii Bendera alisema: “Nimeona kwamba, ndani ya mwezi huu (Juni) watakufa wasanii 20. Huu si utani, ni maono.”
“Ni kweli nasali pale, ni kweli pia nilitumwa na Nabii Bendera nikazungumze na wasanii wenzangu kuhusiana na maono aliyooneshwa.
“Huyo anataka waumini, asidanganye watu. Mungu ninayemwamini anaishi ndani ya nafsi ya mtu. Kama kweli aliona hayo, dawa yake yalikuwa maombi tu, siyo kwenda kupakwa mafuta, tena na yeye mwenyewe,” alisema mchungaji huyo.
MSANII KITALE
“Naamini binadamu kufa ni mipango ya Mungu hakuna anayeongea na Mungu, ninachoamini nabii aliyekuwepo ni Musa tu ambaye alikuwa anatabiri kitu na kikatokea.”
ELIZABETH MICHAEL ‘LULU’
“Kiukweli inatisha na inaogopesha lakini mimi ninasali kwa imani yangu na siwezi kusema utabiri hamna au upo kwani hata kwenye Biblia upo ila siwezi kujua huyu anasema kweli au uongo kwa sababu nabii hana alama.”