MOURINHO: ‘SUAREZ ANAJIRUSHA KAMA YUPO BWAWA LA KUOGELEA!’
>>‘KOSA PEKEE LA REFA HOWARD WEBB NI KUTOMPA KADI SUAREZ!!’
>>BRENDAN RODGERS: “ILIPASWA ETO'O APEWE KADI NYEKUNDU!
Katika moja ya matukio ya Suarez ni pale
 alipokuwa akimfukuza Cesar Azpilicueta ndani ya Boksi na kugongana na 
Samuel Eto'o na hilo limemkera Jose Mourinho aliesema: “Hakuzongwa. 
Suarez alizidiwa maarifa na Azpilicueta ambae alikuwa na Mpira huku 
akitoka nje ya Boksi. Suarez akaamua kujirusha kama vile anadaivu kwenye
 Bwawa la Kuogelea!”
Mourinho aliongeza: “Ni mjanja kwani 
anajua yuko kwenye Boksi na nyuma ya Goli wapo Mashabiki wa Liverpool! 
Lakini Refa Howard Webb alikuwa Mita 10 tu na nadhani kosa pekee 
alilofanya ni kutompa Kadi ya Njano Suarez!”
Tukio hilo lilitokea katika Dakika za 
mwisho za Mechi ambayo Liverpool walitangulia kufunga kwa Bao la Martin 
Skrtel na Chelsea kujibu kwa Bao za Eden Hazard na Samuel Eto'o.
Pia Mourinho alieleza: “Siku zote 
nafurahi kumuona Suarez kwani ana Kipaji, anajituma na ana ari ya 
ushindi. Ni Mchezaji Bora. Lakini Nchi hii ni spesho. Mimi si Muingereza
 lakini nina wajibu kutetea thamani ya Soka hapa. Kitu kimoja bora 
tunacho hapa ni kuwa Watu hawapendi kuhadaa. Ile hali iliyokuwepo kati 
ya yeye na Azpilicueta na Eto'o ni lazima ikome au apewe Kadi za Njano 
kwani si kitu chema kwa Soka letu.”
Suarez, ambae ni Raia wa Uruguay, Msimu 
huu amefunga Bao 19 katika Mechi 14 tangu arejee Kiwanjani akitokea 
kwenye Kifungo cha Mechi 10 kwa kumuuma Meno Beki wa Chelsea, Branislav 
Ivanovic, Mwezi Aprili kwenye Mechi kati ya Liverpool na Chelsea.
Brendan Rodgers atetea!
Hata hivyo, Meneja wa Liverpool, Brendan
 Rodgers, ambae alikuwa Msaidizi wa Jose Mourinho kati ya Miaka 2004 na 
2007 wakati wa himaya ya kwanza ya Mourinho huko Chelsea kwa mara ya 
kwanza, alikuwa na mtazamo tofauti na hasa tukio la Eto’o kumchezea 
faulo Jordan Henderson iliyoleta Frikiki iliyozaa Bao la Skrtel.
Rodgers amedai: “Ilipaswa Eto'o apewe 
Kadi Nyekundu! Najua tumefunga kwa faulo yake lakini ile ni rafu mbaya 
na hakupata hata Kadi ya Njano!”
Kuhusu Suarez, Brendan Rodgers ameeleza:
 “Luis Siku zote atasababisha Mabeki wamvae, ndio maana yuko kiwango cha
 juu Duniani. Kitu ambacho hakutegemea ni kugongwa na Mtu ambae hana 
Mpira. Pale alikuwa akikimbia kumkabili Azpilicueta na Eto'o ana ujanja 
wa Mtaani, alifanya safi, alimziba Suarez. Siku nyingine unaweza kutoa 
ile iwe Penati kwa sababu amemzuia!”
Brendan Rodgers alimalizia: “Ni dhahiri, Mourinho atamtetea Mchezaji wake na mimi nitamtetea wangu!”
RATIBA MECHI ZIJAZO:
[Saa za Bongo]
Jumatano Januari 1
1545 Swansea v Man City
1800 Arsenal v Cardiff
1800 Crystal Palace v Norwich
1800 Fulham v West Ham
1800 Liverpool v Hull
1800 Southampton v Chelsea
1800 Stoke v Everton
1800 Sunderland v Aston Villa
1800 West Brom v Newcastle
2030 Man United v Tottenham
MSIMAMO:
| NA | TIMU | P | GD | PTS | 
| 1 | Arsenal | 19 | 19 | 42 | 
| 2 | Man City | 19 | 33 | 41 | 
| 3 | Chelsea | 19 | 16 | 40 | 
| 4 | Everton | 19 | 13 | 37 | 
| 5 | Liverpool | 19 | 21 | 36 | 
| 6 | Man United | 19 | 10 | 34 | 
| 7 | Tottenham | 19 | -2 | 34 | 
| 8 | Newcastle | 19 | 5 | 33 | 
| 9 | Southampton | 19 | 6 | 27 | 
| 10 | Hull | 19 | -1 | 23 | 
| 11 | Swansea | 19 | -1 | 21 | 
| 12 | Stoke | 19 | -11 | 21 | 
| 13 | Aston Villa | 19 | -7 | 20 | 
| 14 | Norwich | 19 | -16 | 19 | 
| 15 | West Brom | 19 | -5 | 18 | 
| 16 | Cardiff | 19 | -15 | 18 | 
| 17 | Crystal Palace | 19 | -16 | 16 | 
| 18 | Fulham | 19 | -22 | 16 | 
| 19 | West Ham | 19 | -10 | 15 | 
| 20 | Sunderland | 19 | -17 | 14 | 
 
 
 
 
 
 
