Header Ads

WANAFUNZI WA FANI YA UANDISHI WA HABARI NA UTANGAZAJI ARUSHA WAKAMILISHA RASIMU MPYA YA KATIBA.



Mgeni rasmi ambaye ni mwalimu mlezi wa chuo cha Uandishi wa Habri na Utangazaji Arusha kushoto 











Mgeni Rasmi akikabidhiwa rasimu mpya ya chuo cha A.J.T.C

Rais wa chuo hicho Bw George Silange akishikana nmkono na katibu wa Rasimu hiyo Bi Emelda Stephano
Mwenyekiti wa katiba katika Chuo Cha uanadishi wa Habari na Utangazaji Arusha Bw,Oska Samba akimkabidhi mgeni Rasmi rasimu mpya ya katiba.

Hatimaye wanafunzi katika chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Arusha(A.J.T.C)leo wamekabithi rasimu mpya ya katiba iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu kwa kipindi kirefu na wanafunzi ili kupata muongozo wa katiba.
Rasimu hiyo ambayo inapelekea kupatikana kwa katiba mpya imetajwa kama muhimili mkuu wa uongozi kwa kutoa ufafanuzi na muongozo mkuu wa madaraka pamoja na mipaka kwa waalimu pamoja na serikali ya wanafunzi na kila mmoja kupata haki zake za kimsingi.
Akikabidhi rasmi hiyo ya katiba mbele wa mgeni rasimi mwenyekiti wa tume hiyo Bw,OSKA SAMBA amesema kuwa katiba mpya itato majibu ya kila swali ambalo wanachuo wamekuwa wakijiuliza na kudai kudai  ni hatua kubwa imefikiwa na tume yake kuweza kukamilisha rasimu hiyo ya awali.
Amesema katika uchambuzi wa rasimu ya katiba hiyo ambayo itafanyika kuanzia jumanne ya tarehe 28january 2014 utafanyika katika hali ya amani na upendo na wala sio kwakuwekeana vinyongo kutokana na awali kuonekana kuleta mvutano na baadhi ya wakufunzi chuoni hapo juu ya utaratibu wa utoaji na ukusanyaji maoni  uliofanyika mwezi mmoja uliopita.
Pamoja na hayo amesema licha ya kukamilisha rasimu hiyo pia zipo changamoto ambazo wamekumbana nazo ikiwemo ukosefu wa fedha,baadhi ya wajumbe kujiuzulu,na kukimbia pamoja na kukatishwa tamaa na baadhi ya watu wasiopenda maendeleo.
Kwa upande wa mwalimu mlezi wa Chuo hicho cha Uandishi wa habari na utangazaji Arusha ambaye pia alikuwa mgeni rasmi Bw ANDREA NGOBOLE Ameipongeza tume ya katiba pamoja na serikali ya wanafunzi kupitia kwa Raisi wa Chuo hicho Bw George Silange na kusema kuwa wamekuwa wa kwanza kuweza kuafanikisha rasimu hiyo ikiwa ni moja ya ahadi zao.
Amesema chuo hicho kwa miaka tisa akijawahi kuwa na katiba ya serikali ya wanafunzi na badala yake ilikuwa ikitumika ya uongozi wa chuo na kudai na kuwataka wanafunzi hao kuipokea rasimu hiyo kwa furaha na kuhakikisha katiba mpya inapatikana.
Powered by Blogger.