Header Ads

MCHUNGAJI MSIGWA ATAKIWA KUELEZA ZILIKO FEDHA ZA VISIMA VYA MAJI ZILIZOTOLEWA NA SABODO



Katibu wa CCM Manispaa ya Iringa, Hassan Mtenga katika uzinduzi wa kampeni hiyo
CHAMA cha Mapinduzi (CCM) Iringa Mjini kimezindua kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Nduli huku kikimtaka mbunge wa jimbo la Iringa Mjini, Mch Peter Msigwa (Chadema) kuwaeleza wananchi ziliko fedha zilizotolewa na Mustafa Sabodo kwa ajili ya kuchimba visima vya maji.

Baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2010, Sabodo aliahidi kutoa fedha kwa ajili ya kuchimba visima 200 kwenye majimbo yote yanayoongozwa na chama hicho, alisema Katibu wa CCM Manispaa ya Iringa, Hassan Mtenga kwenye mkutano huo.

“Muulizeni Msigwa fedha hizo ziko wapi, mbona jimbo la Iringa Mjini hakuna kisima hata kimoja kilichochimbwa,” alisema katika mkutano huo ambao Frederick Mwakalebela alishangiliwa kwa nguvu kubwa na mamia ya wananchi waliohudhuria huku wakimwita jembe la Uchaguzi Mkuu ujao.

Pamoja na visima vya Sabodo, Mtenga aliwataka wananchi wa kata ya Nduli na jimbo la Iringa Mjini kumuuliza mbunge huyo ahadi aliyotoa wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu uliopita wa mwaka 2010 ya kuweka wakili ofisini kwake kwa ajili ya kutetea wananchi masikini imefia wapi.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa Amani Mwamwindi alisema tangu Mchungaji Msigwa awe mbunge wa jimbo hilo miaka mitatu iliyopita, rekodi katika halmshauri yao zinaonesha amefanya mambo mawili tu kwa wakazi wa jimbo la Iringa Mjini.

Bashir Mtove, mgombea udiwani kata ya Nduli (CCM) akinadiwa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa Amani Mwamwindi
Alizitaja kazi zilizofanywa na mbunge huyo kuwa ni kutoa vitanda 30 vinavyotumia umeme na baiskeli za miguu miwili 12 katika hospitali ya Manispaa ya Iringa na kugawa mipira kwa timu za mpira katika kata zote za jimbo la Iringa Mjini.

Alisema vifaa vilivyotolewa na Mchungaji Msigwa katika hospitali hiyo vilitolewa na asasi isiyo ya kiserikali ya Reach Out Tanzania for Charity (ROTC).

Viti na vitanda vilivyokabidhiwa na Mchungaji Msigwa katika hospitali hiyo
Naye Katibu Mwenezi wa CCM Manispaa ya Iringa, Thobias Kikula alisema katika mkutano huo kwamba katika moja ya ahadi zake kwa wapiga kura wa jimbo la Iringa Mjini, Mchungaji Msigwa aliahidi kutenga Sh Milioni 12 kila mwaka kutoka katika familia yake kwa ajili ya kuchangia shughuli mbalimbali za maendeleo katika jimbo hilo.

“Muulizeni tangu kwa miaka mitatu mfululizo amechangia shughuli gani za maendeleo kwa kutumia fedha hizo,” alisema.
Kikulacho (kulia)
Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kusini, Medrad Kigola alisema katika mkutano huo kwamba “ ni hatari kuwa na mbunge ambaye akienda nje ya nchi kazi yake ni kushangaa maghora na akirudi nchini kujitapa kwa safari zake zisizo na tija.”
 
Mbunge Kigola akinena

“Muulizeni Mchungaji Msigwa ametembelea nchi ngapi duniani na katika zira zake hizo wakazi wa jimbo la Iringa mjini wamenufaika vipi?” alisema.

Akimnadi mgombea udiwani wa kata hiyo Bashiri Mtove, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa aliwataka wakazi wa Nduli kumpigia kura ili amalizie utekelezaji wa Ilani ya CCM katika kata hiyo.

 “Kuna mradi wa maji wa Sh Milioni 800 katika kata hii; umekuja ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya CCM, barabara ya Kigonzile inajengwa kwa Sh Milioni 102 na daraja katika barabara hiyo linajengwa kwa Sh Milioni 54,” alisema.

 Alisema wakati madiwani wa halmshauri ya Manispaa ya Iringa wakipeleka maendeleo kwa wananchi wa jimbo la Iringa Mjini, Mchungaji Msigwa anaendelea kupiga kelele kuhusu tembo na faru.

“Muulizeni kama jimbo la Iringa Mjini lina hao wanyama?; ni kweli wanyama hao ni rasilimali ya Taifa na ni muhimu wakalindwa, lakini kuendelea kuwa na mbunge ambaye hashughuliki na matatizo ya wapiga kura wake na badala yake anashughulika na mambo ya kitaifa ni hatari kwa maendeleo ya mji wetu,” alisema.

Alisema mbali na bungeni, maendeleo ya watu wa jimbo la Iringa Mjini ayanajadiliwa katika vikao vya baraza la madiwani ambalo yeye sio muhudhuriaji mzuri.

 “Amenza kuhudhuria vikao hivyo mwaka jana, katika kipindi cha miaka miwili ya mwanzo wa ubunge wake halikuwa haptikani,” alisema.

Mwakalebela naye alipata fursa ya kuzungumza

Jesca akiwapagaisha wananchi wa kata ya Nduli kwa sera ya amani

 
Wengine waliohutubia mkutano huo ni pamoja na Mwakalebela aliyewasihi wana Nduli kutofanya makosa kulinda maslai ya kata hiyo na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu aliyewataka vijana wajiepushe na kampeni za uvunjaji wa amani zinazofanywa na baadhi ya wanasiasa.
Powered by Blogger.