Header Ads

MGOMO WA WAFANYABISHARA IRINGA WAENDELEA, WATOA MASHARTI YA KUFUNGUA MADUKA YAO

sehemu ya wafanyabishara hao




Mwenyekiti wa TCCIA, Mwakabungu akifafanua baadhi ya mambo
WAFANYABIASHARA walioko katika mgomo wa kutumia mashine za kodi za kielektroniki (EFD) wa mjini Iringa wamekubaliana kuendelea na mgomo wao mpaka pale serikali itakaposikiliza kilio chao.
Mapema hii leo wafanyabiashara hao walikubaliana kufunga maduka yao wakipinga matumizi yam shine hizo zinazouzwa kwa kati y ash 600,000 na sh 800,000.
Katika kikao chao walichofanya kati ya saa nane mchana hadi saa 11 jioni ya leo, wafanyabiashara hao wamesema ni bora wapate hasara katika biashara zao kuliko kuendelea kukubalina na kila kitu kinachoamuliwa na serikali.
Kikao hicho kilifanywa kwa urataibu wa Chemba ya Biashara, wenye Viwanda na Kilimo (TCCIA) Mkoa wa Iringa.
Hatufungui maduka mpaka tutakapokutana na Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania mkoani hapa, wabunge wote wa Iringa Mjini, Mkurugenzi  na Madiwania wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, alisema mmoja wao aliyejitambulisha kwa jina la Lusajo.
Lusajo alisema mshine hizo zimegeuka kero kwa wafanyabishara wengi na akashangaa sheria ya kukwepa kutoa risiti kwa wateja ikiwalazimu kulipa faini ya Sh Milioni 3.
“Yaani mfanyabiashara anayeshindwa kutoa risiti kwa kuuza pakti ya sigara, peni au karatasi analipa faini sawa na anayekwepa kutoa risiti kwa bidhaa zinazojaa kontena nzima,” alisema Mzee Kaundama.
Alisema sheria hiyo haiwatendei haki wafanyabishara wengi na imekuwa ikitengeneza mazingira ya rushwa kwa maafisa wa TRA.
Alisema inawezekanaje kwa mfanyabiashara mwenye mtaji wa Sh Milioni moja akalipa kodi ya mapato asilimia 30, Ongezeko la Kodi ya Thamani asilimia 18 na akafanya marejesho kwa riba ya asilimia 25 ya mkopo aliochukua kutoka katika taasisi za fedha.
“Hakuna mfanyabishara anayekataa kulipa kodi, lakini kwa mazingira hayo mfanyabishara huyo anayehitaji mazingira rafiki na serikali yake atabakiwa na nini baada ya kolipa kodi hizo, kodi ya pango na gharama zingine za uendeshaji?” alisema.
Mwenyekiti wa TCCIA, Lucas Mwakabungu alisema chemba yao iko pamoja na wafanyabishara hao na akaishangaa serikali kwa kuwa na lundo la kodi kwa wafanyabishara wake.
“Tuna kodi zaidi ya 24 katika nchi hii, tofauti na wenzetu wa Rwanda wenye kodi zisizozidi 12,” alisema.
Hata hivyo alisema shida ya nchi hii sio serikali, ni tabia ta watendaji wabovu wanaopaswa kuwajibishwa lakini wanaendelea kulindwa.
“Yalipoanzishwa matumizi ya mashine hizo hakukuwa na maoni kutoka kwa wadau, leo maamuzi yaliyofanywa na wachache yanawathiri wao, serikali na wananchi wanaowatumikia,” alisema.
Alisema serikali inatakiwa kuwafukuza kazi watu waliohusika na mapendekezo ya uanzishaji wa matumizi ya mashine hizo kwakuwa mchakato wake haukufuata taratibu shirikishi.
Akizungumzia msimamo wa TCCIA, Mwakabungu alisema haihafiki matumizi yake kwasasa kwa kuwa hayakuwa na maandalizi na sasa yanaleta adhabu kwa wadau.
Powered by Blogger.