Header Ads

MWENYEKITI WA CCM MKOA WA DAR ES SALAAM APANDISHWA KIZIMBANI

3a
Madabiba
OFISA Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Tanzania Pharmaceutical Industries (TPI) Ltd, Ramadhani Madabida amefikishwa mahakamani akidaiwa kusamba dawa bandia za kupunguza makali ya virusi vya Ukimwi (ARV).
Madabida na wenzake watano, wakiwemo watumishi wa Boahari Kuu ya Dawa (MSD), walipandishwa kizzimbani Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu Dar es Salaam.
Kwa kusambaza dawa hizo feki, Madabida ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam na wenzake watano wanadaiwa kuisababishia serikali hasara ya Sh Milioni 148.
Washitakiwa wengine katika kesi hiyo namba tano ya uhujumu uchumi ni wafanyakazi wa TPI, Mkurugenzi wa Uendeshaji Seif Shamte, Meneja Masoko Simon Msofe na Mhasibu Msaidizi Fatma Shango.

Watumishi wa MSD ni Meneja Udhibiti Ubora, Sadiki Materu na Ofisa Udhibiti Ubora, Evans Mwemezi.
Powered by Blogger.