Header Ads

MKE WA MTU AZAA NJE YA NDOA NA KUTUPA KICHANGA CHOONI IWAMBI MBEYA

Rukia Fungameza (20), mtuhumiwa nayaetuhumiwa kutupa kichanga chooniAdd caption

Choo alichotupwa kichanga huyo

Akinamama wakisikitika kwa uchungu


Mwenyekiti wa Mtaa, Juma Mbuza (mwenye fulana ya bluu) akiwa na Balozi wa mtaa huo kushoto pamoja na mashuhuda wengine wakijadili udhalimu huo


Mtuhumiwa akipelekwa Polisi



Rukia Fungameza (20), mkazi wa mtaa wa Ilembo Kata ya Iwambi anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya kwa tuhuma za kutupa chooni kichanga cha kiume na kusababisha kifo chake.
Mwenyekiti wa mtaa huo Juma Mbuza alisema Februari 18, mwaka huu walianza kumtilia shaka mtuhumiwa huyo baada ya kuonekana hana ujauzito huku kukiwa hakuna taarifa zozote za kujifungua.
Alipoulizwa kulikoni, mtuhumiwa huyo alidai kajifungua salama huku akiwaondoa hofu majirani zake.
Tetesi zilizotilia shaka ujauzito wa mtuhumiwa huyo zilimlazimu Mwenyekiti huyo, kumtafuta Balozi Daud Dule wa mtaa anaoishi mtuhumiwa huyo ili ajue ukweli wa tukio hilo.
Alipobanwa, mtuhumiwa huyo alikiri kujifungua salama lakini  Februari 18 alilazimika kukitupa kichannga chake chooni kwa kuwa mimba haikuwa ya mme anayeishi naye.
Baada ya kukiri kufanya unyama huo, mtuhumiwa alikamatwa na wananchi na kufikishwa kituo cha Polisi Iyunga.
Baadhi ya mashuhuda akiwemo mama Emilly Amoni na Paulo Mbawala wamelaani vikali kitendo kilichofanywa na mwanamke huyo kwani wamedai ni cha kinyama na ni cha kwanza mtaani kwao hivyo wanaomba sheria iweze kuchukua mkondo wake ili kukomesha kabisa vitendo vya kikatili vya aina hiyo.
Na Ezekiel Kamanga
Mbeya yetu
Powered by Blogger.