Header Ads

Siku za kwenda Brazil Kombe la Dunia ziko ukingoni

FIFA-World-Cup-2014-Brazil
Ni siku 100 tu, ni vigumu kuamini kuwa iko karibu. Inaonekana kama jana tu kwamba Brazil imethibitishwa kuwa muandaaji wa FIFA World Cup 2014. Nakumbuka msisimko niliohisi na kuona kuwa nchi yangu inaenda kwenye hatua muhimu ya mpira katika Dunia hii.

Hata ingawa mimi sitakuwa uwanjani, lakini nimeanza kupata vipepeo tumboni kama ambavyo nilikuwa nikikaribia mechi kubwa. Baada ya yote kumalizika FIFA World Cup, itakuwa ni ya aina ya mwisho kwa Brazil, tofauti na kujitangaza yenyewe kimataifa. Uangalizi utakuwa juu yetu na ni nafasi kubwa kwetu kwa kuionyesha Dunia umuhimu kuhusu Brazil na watu wa Kibrazil walivyo.

Wakati wa Kombe la Dunia la Olimpiki 2016 itakayofanyika Brazil, tutakuwa na nafasi ya kuionyesha Dunia jinsi tunavyo penda michezo na vilevile tulivyo na nguvu katika uchumi wetu. Brazil ni kiongozi mkubwa Duniani kiteknolojia na kiongozi mkubwa wa uzalishaji wa Nyama, madini na mzalishaji mkubwa wa soya duniani. Ni karibu sasa maelfu ya watalii na waandishi wa kigeni watafika kwenye mlango wetu ulio wazi kujionea na kugundua uhalisia wa Wabrazili.
Ingawa Brazili ni nchi kubwa kijamii, lakini tumefanya mambo mengi ya kukabiliana na matatizo katika miaka ya hivi karibuni. 

Tuna utaifa tofauti lakini tuna umoja mzuri kijamii na kimaendeleo katika ubunifu wa juu. Ni nchi iliyojaliwa watu wenye uwezo mkubwa kiakili na inawatu wengi wenye vipaji vikubwa katika michezo kama Neymar anavyocheza na maajabu yake ya kuchezea mpira . Vilevile mziki wa Tom Jobim na sayansi aliyoipata kutoka kwa Miguel Nicolelis, kama utafiti waliofanya na kupata matumaini kuwa siku moja mifupa ya binadamu inaweza kutembea tena.
estadios2014
Brazili ni nchi nzuri sana, na ni nchi iliyobarikiwa kuwa na hali ya asili nzuri. Watalii wote watakaofika Brazil wakati wa Kombe la Dunia wajiandae kukutana na hali ambayo hawataisahau na hawajawahi kuiona. Vilevile watafurahia kutembelea fukwe za kusini na kujionea misitu na mto wa Amazon, milima katika mji wa Rio de Janeiro ambayo ni sehemu muhimu sana kwa watalii. Naamini kila mtalii ataondoka Brazil akiwa na kumbukumbu nzuri katika maisha yake yote.
Powered by Blogger.