Header Ads

WAVAMIZI NA WAARIBIFU WA VYANZO VYA MAJI WATAKIONA CHA MOTO.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Nyirembe Munasa (wakwanza kulia) akiwasili katika chanzo cha maji kilichopo eneo la Loruvani wilayani hapo kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa uzio wa kulinda chanzo hicho kisiharibiwe ikiwa ni moja kati ya shughuli zinazofanywa na Mamlaka ya Maji safi na maji taka Arusha (AUWSA) katika maadhimisho ya wiki ya maji iliyoanza jana kimkoa.Wakwanza kushoto ni Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka hiyo Bi Sifa Swai.Picha na Joseph Richard\                            
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Nyirembe Munasa (Katikati) akihutubia wananchi wa eneo la Loruvani juu ya umuhimu wa kutunza vyanzo vya maji ili upatikanaji wake uwe endelevu ,kabla ya shughuli ya kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa uzio wa kulinda chanzo hicho kisiharibiwe ikiwa ni moja kati ya shughuli zinazofanywa na Mamlaka ya Maji safi na maji taka Arusha (AUWSA) katika maadhimisho ya wiki ya maji iliyoanza jana kimkoa.Wapili kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa AUWSA,Fabian Maganga,Wakwanza kulia ni Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka hiyo Bi Sifa Swai.Picha na Joseph Richard                          





Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Bw Nyirembe Munasa  Amesema serikali itwachukulia hatua kali za kisheria watu wanaovamia na kuaribu vyanzo vya maji ili kukomesha tabi hiyo pamoja na kuboresha vyanzo hvyo.
Ameyasema hayo wakati akizingua miradi ya maji ya visima viwili pamoja na kujengea usio kulinda vyanzo hivyo katika wiki ya maji  na nishati Mkoani Arusha katika Wilaya ya Arumeru Kijiji cha Loruvani yaliyosimamimiwa na mamlaka ya Maji Arusha AUWSA ambapo amewataka wavamizi kuacha tabia hiyo mara moja
Bw Nyirembe amesema maji ni uhai hivyo kuahidi kuwachukulia hatua kali za kisheria watu wote ambao watahusika katika kuhujumu miradi hiyo ya maji kwakuwa sheria zipo wazi kwa yeyote atakaye kiuka taratibu na sheria za kulinda vyanzo hivyo muhimu vya maji.
Pamoja na hayo amesema serikali peke yake haiwezi kupambana na matukio hayo hivyo kuwataka wananchi pamoja na Taasisi mbalimbali kushirikiana kikamilifu ili kuhakikisha wanatatua tatizo la uharibifu wa vyanzo vya maji pamoja na kutatua tatizo la maji.
Hata hivyo  Mkurugenzi mtendaji wa mamlaka hayo Mkoa wa Arusha Bw Fabia Maganga amesema wanakabiliwa na changamoto mbalimbali kama vile utunzaji wa vyanzo vya maji pamoja na ongezeko la  Watumia wa huduma hiyo hivyo kusababisha kuwapo na uhaba mkubwa wa maji safi na salama.
Kauli mbiu katika wiki ya Maji na Nishati  ni Uhakika wa maji na Nishati kwakuwa mategemezi ya maji katika sekta ya nishati ni makubwa hivyo kuwataka wananchi kuona ulazima wa kutunza na kulinda vyanzo vya maji
Powered by Blogger.