Header Ads

NAPE AMJIBU DK.SLAA

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na Waandishi wa Habari katika ukumbi wa Sekretarieti,Makao Makuu ya CCM Ofisi Ndogo Lumumba,ambapo aliwaeleza kuwa Kamati Kuu imemteua  Ndugu Philipo Mangula kuongoza Timu ya Kamati Maalum ya CCM itakayoandaa Ilani ya CCM katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa  pia Kamati Kuu imemteua Ndugu Adam Kimbisa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Uhuru Media tarehe 16 Julai 2014.

Jana Julai 15, 2014 Katibu Mkuu wa Chadema Dk. Wilbroad Slaa alitoa shutuma kadhaa dhidi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Katika shutuma hizo, Dk. Slaa aliwatangazia wanahabari kuwa wamefanikiwa kudaka mawasiliano ya siri pamoja na waraka wa Chama Cha Mapinduzi uliodai kuwa umeandaliwa na Kamati maalumu na kuuwasilisha kwa Katibu Mkuu wa CCM ili aupeleke kwa Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete ikiwa ni taarifa ya mwenendo wa Bunge Maalum la Katiba.
Ukweli ni kwamba taarifa za hicho ambacho Dk. Slaa amekiita ni waraka kutoka kwa Kamati Maalum kuhusu mwenendo wa Bunge Maalum la Katiba ni uzushi mtupu na unadhihirisha namna walivyo wavivu wa kufikiri kiasi cha kuanza kutunga andiko na kutangaza wenyewe kwa jina la waraka.
Jambo moja wanaloonekana kulimudu Chadema ni uwezo wao wa kutunga uongo na kupanga maandamano. Na hii ndio siri ya Watanzania kuwakataa kila kukicha na ndio siri ya kufa kwa chama hicho, kwani njia ya muongo ni fupi.
Dk. Slaa na Ukawa lazima wajue kuwa hesabu waliyoipiga katika kujitafutia umaarufu kupitia mchakato wa Katiba mpya umeshindwa kufanikiwa, hivyo kubakia wakitapatapa bila hoja hakutawasaidia.
Ukweli ni kwamba CCM haina haja ya kuhofia mchakato wa Katiba mpya kwa namna yoyote, kwa sababu Mwenyekiti wake aliuanzisha akijua umuhimu wake kwa wakati wa sasa hasa ikizingatiwa kuwa tayari Katiba tuliyonayo ishatufikisha mahali pa kuridhisha kwa miaka hamsini iliyopita.
Kikubwa ni kwa Watanzania kutokubali upotoshaji na uzushi wa baadhi ya viongozi akiwemo Dk. Slaa, badala yake wananchi wajikite katika kufuatilia na kushiriki katika awamu mbili zilizobakia kwa kuwa ndizo zitakazofanikisha kukamilika kwa mchakato wa Katiba mpya bila matatizo.
Aidha, Dk. Slaa ametumia nafasi hiyo na kujigeuza kuwa msemaji wa CCM kwa kuanza kutangaza juu juu bila takwimu uhusiano wa CCM na taasisi ya Friederich Herbert Stuftung (FES). Suala la uhusiano wa FES na CCM si la namna ambayo Dk. Slaa anataka kulielezea. Bali uhusiano wa karibu kati ya Rais wa zamani wa Ujerumani na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere uliojenga mahusiano makubwa ya kisiasa miongoni mwao.
Kwa kuwa busara ya Dk. Slaa ni kutunga uongo nalo hilo kwake limekuwa ni utetezi wa misaada ya masharti magumu wanayopokea wao kutoka nje bila kuwaambia Watanzania malipo ya misaada hiyo.
 
Powered by Blogger.