Header Ads

WAUMINI NA WACHUNGAJI WA KANISA LA MOROVIANI MBEYA WAFUNGA KANISA KUSHINIKIZA ASKOFU WAO AJIUZULU

 
 Baadhi ya wachungaji na waumini wa kanisa la Moravian jimbo kuu la kusini magharibi wamefunga kanisa kuu la jimbo hilo jijini Mbeya wakishinikiza askofu mkuu wa jimbo la kusini magharibi, mchungaji Alinikisa Cheyo ajiuzulu kutokana na kukiuka katiba ya kanisa lao.
-
Ni wachungaji na waumini wa kanisa la Moravian jimbo kuu la kusini magharibi ambao wameamua kufunga geti la kanisa pamoja na ofisi ya baba askofu Alinikisa Cheyo wakishinikiza askofu huyo ajiuzulu na hapa baadhi ya wachungaji hao wanaelezea sababu ya wao kuchukua uamuzi huo.
 
Akizungumzia tukio hilo, makamu mwenyekiti wa kanisa  hilo, mchungaji Zacharia Sichone amesema waliofunga kanisa hilo ni watovu wa nidhamu kwa sababu wanajua kuwa kanisa linaendeshwa kwa taratibu na katiba waliyojiwekea.
 
Ili kuepusha uvunjifu wa amani katika eneo hilo, imembidi mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Mbeya ambaye pia ni mkuu wa wilaya hiyo, Dk. Norman Sigalla kuingilia kati na kuwataka wachungaji hao kufungua kanisa hilo huku akiwaahidi kuwa ufumbuzi wa mgogoro wao utapatikana kwenye kikao kitakachofanyika kesho kati ya uongozi wa kanisa hilo na kamati yake ya ulinzi na usalama.
Powered by Blogger.