Header Ads

Viongozi CHADEMA waazimia kutompa ushirikiano mkuu wa wilaya ya Njombe.


Viongozi wa chama cha Demokarasia na Maendeleo wilaya ya Njombe wametoa maazio ya kuto fanya kazi na mkuu wa wilaya ya Njombe ,Bi  RUTH MSAFIRI kwa kile walichodai kuwa alimdhalilisha  mwenyekiti wa mtaa wa Buguruni kwa kumchapa makofi  February 28 mwaka huu akiwa ofisini kwake.


Uongozi wa chama hicho wilaya umekuja na tamko la pamoja na kumtaka mkuu wa wilaya a N jombe kuomba radhi ndani ya siku 7 na la sivyo hatapewa ushirikiano na vingozi wote wa chama hicho wakiwemo Wenyeviti wa Mitaa na Madiwani.
 
Akizungumza na waandishi wa habari Mwenyekiti wa wenyeviti wa chama cha CHADEMA, Bw.BARASION MGAYA amemtaka kiongozi huyo  kuheshimu uongozi uliowekwa na wananchi.
 

Kwa upande Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi, RUTH MSAFIRI amekana kumpigia mwenyekiti huyo na kusisitiza   aliamuru vyombo vya ulinzi kumuweka ndani kwa masaa 48 kwa kile alichodai kuwa ali toa lugha ya matusi dhidi yake.
Powered by Blogger.