Header Ads

RIBERY NDIE MCHEZAJI BORA FRANCE 2013!

ABWAGA POGBA NA MATUIDI!!
KOCHA BORA FRANCE NI RUDI GARCIA!!
FRANCK_RIBERYFranck Ribery, ambae ametinga kwenye Listi ya Mwisho ya Wagombea ya Tuzo ya Mchezaji Bora Duniani, 2013 Ballon d'Or, ametangazwa kuwa ndie Mchezaji Bora wa France kwa 2013.
Jarida maarufu la Nchi hiyo, France Football, ambalo ndio walioanzisha Ballon d'Or Mwaka 1956 ili kumpata Mchezaji Bora Ulaya na kuanzia Mwaka 2010  wakashirikiana na FIFA kumpata Mchezaji Bora Duniani na kumpa Tuzo iitwayo FIFA Ballon d'Or, ndio pia hutoa Tuzo ya Mchezaji Bora wa France.
Ribery, anaechezea Klabu Bingwa ya Ulaya na Germany, Bayern Munich, amewabwaga Kiungo wa Juventus Paul Pogba na yule wa Paris St Germain, Blaise Matuidi, katika Kura iliyopigwa na Wachezaji wa zamani na wa sasa wa France.
Hii ni mara ya 3 kwa Ribery kutwaa Tuzo ya Mchezaji Bora wa France na mwenyewe amesema nia yake ni kuivunja Rekodi ya Thierry Henry alietwaa Tuzo hiyo mara 5.
Mwaka huu, Ribery aliweza kuisaidia Klabu yake Bayern Munich kutwaa UEFA CHAMPIONZ LIGI, Bundesliga na German Cup, na pia yupo kwenye kinyang’anyiro cha Tuzo ya Mchezaji Bora Duniani, 2013 Ballon d'Or, akichuana na Cristiano Ronaldo na Lionel Messi na Mshindi wake atatajwa Januari 13.
Nae Kocha wa AS Roma, Rudi Garcia, ambae alijiunga na Klabu hiyo ya Serie A huko Italy mwanzoni mwa Msimu akitokea Klabu ya France Lille, na ambe hajafungwa katika Mechi 15 za Ligi, ndie ametangazwa kuwa ndie Kocha Bora wa France kwa 2013 baada ya Kura iliyopigwa na Makocha wa sasa na zamani huko France.
Powered by Blogger.