Header Ads

BORA KWA DESEMBA-LIGI KUU ENGLAND: NI PELLEGRINI & SUAREZ!!

PELLEGRINI-KIDOLEBOSI wa Manchester City Manuel Pellegrini ndie  ametajwa kuwa Meneja Bora wa Ligi Kuu England kwa Desemba pamoja na Straika wa Liverpool Luis Suarez alietwaa Tuzo hiyo kwa upande wa Wachezaji.
Tuzo hizi hutolewa na Wadhamini wa Ligi Kuu, Barclays.
Pellegrini, Mwenye Miaka 60 na Raia wa Chile ambae alichukua wadhifa wake mwanzoni mwa Msimu baada ya kutimuliwa Roberto Mancini, ametwaa Tuzo hii kwa mara ya kwanza baada ya kuiongoza Man City kutofungwa katika Mechi 7 za Ligi kwa Mwezi Desemba.
Man City walishinda Mechi 6 na kutoka Sare ya Bao 1-1 na Southampton na miongoni mwa ushindi wao ni dhidi ya Arsenal na Liverpool.SUAREZ
Pellegrini ametwaa Tuzo ya Desemba kwa kuwashinda Meneja wa Manchester United David Moyes, wa Chelsea Jose Mourinho na wa Everton Roberto Martinez.
Kwa Msimu huu wa 2013/14, Mameneja waliotwaa Tuzo za kila Mwezi tokea Agosti ni Brendan Rodgers, Arsene Wenger, Mauricio Pochettino na Alan Pardew.
Nae Straika wa Liverpool, Luis Suarez, ametwaa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Barclays  Ligi Kuu England kwa Mwezi Desemba baada ya kuweka Rekodi ya kuwa Mchezaji pekee aliefunga Bao 10 katika Ligi Kuu ndani ya Mwezi mmoja.
Suarez alianza Desemba kwa kushindwa kufunga katika kipigo cha Liverpool cha Bao 3-1 toka kwa Hull City lakini akapiga Bao 4 wakati wanaifumua Norwich City Bao 5-1 Uwanjani Anfield na kisha kufnga Bao 2 kila Mechi walipozishinda West Ham, Tottenham na Cardiff.
Suarez ametwaa Tuzo ya Desemba kwa kuwabwaga Wachezaji watatu wa Man City, Alvaro Negredo, Vincent Kompany na Yaya Toure, na pia Ross Barkley wa Everton na Theo Walcott wa Arsenal.
Powered by Blogger.