Header Ads

SMZ YASHAURIWA KUIMARISHA HALI YA USALAMA WA ENEO LA NYARAKA

Na Miza Kona   -Maelezo Zanzibar       

Serikali ya Mapinduzi imeshauriwa kuimarisha hali ya usalama wa eneo la Nyaraka kwa kuweka kamera za kuangaza usalama kwa ukaribu CCTV ili kuepusha wizi  usitokee katika Idara hiyo.

Akiwasilisha Muhtasari wa Ripoti ya Kudumu ya Katiba, Sheria na Utawala ya Baraza La Wawakilishi kwa mwaka wa Fedha 2013/2014 Mwenyekiti wa Kamati hiyo Ussi Jecha Simai amesema kuwekwa vyombo vya usalama katika idara hiyo kutasaidia kuepusha kuibiwa kwa nyaraka za Taifa na kuipatia hasara nchi.

Aidha amesema Kamati imesikitishwa na na taarifa za wizi wa nyaraka muhimu uliotokea katika Idara na kusisitiza kuwekwa kwa vyombo vya CCTV ili kuweza kubaini wizi huo unapofanyika.  Pia Kamati hiyo wameomba serikali kupitia vyombo vyake usalama kufanya uchuzi wa tukio hilo kwa kila aliyehusika na wizi wa nyaraka kuchukuliwa hatua za kisheria.

Hata hivyo Kamati hiyo imeitaka serkali kuandaa mpango wa kuzifanyia ukaguzi Nyaraka zote  zikiwemo Ofisi ya Vizazi na Vifo pamoja na Wakfu na baada ya muda na ripoti yake ipelekwe katika Baraza ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Wizara.

“Hivi sasa Idara ya Nyaraka imefanywa kama vile ni eneo la kuhifadhia vitu vya kale visivyohitajika tena, eneo lenyewe lipo katika hali hatarishi kiusalama, jengo finyu,halitoshelezi kuhifadhi kwa ufanisi nyaraka nyingi zilizomo”,alieleza. 

Aidha alifahamisha kuwa ustawi wa kiafya kwa wafanyakazi wa Taasisi hiyo upo katika hali ya hatari kutokana na mazingiramagumu  wanayofanyia kazi  kwa kukosa vifaa muhimu ikiwemo ukosefu wa vipoza hewa katika vyumba vya kuhifadhia Nyaraka.

Akichangia Ripoti ya Kamati hiyo Mwakilishi wa Jimbo la Kitope Makame mshimba Mbarouk amesema wizi wa nyaraka umesababishwa kudharauliwa na kutothaminiwa kwa nyaraka za asili pamoja na ukosefu wa vifaa muhimu wa kuchunguza na kubaini wizi unafanyika  hivyo serikali ichukuwe  hatua za kisheria kwa yoyote atakaehusika na wizi huo.

Aidha ameiomba serikali kuanzisha Mahakama za wawekezaji ambazo zitaweza kutekeleza kazi zake ili kuepusha unyang’anyi wa ardhi pale wanapokuja kuwekeza na kupata haki zinazostahiki.   
            
IMETOLEWA NA IDARA YA HABRI MAELEZO                   
Powered by Blogger.