Header Ads

MAN UNITED: “HAMNA DILI NA NDIO MAANA HATUJATANGAZA!”

ROONEY_KIDOLE_JUULEO huko England zimezagaa ripoti  kuwa Straika wa Manchester United na England, Wayne Rooney, amesaini Dili mpya ambayo ni rekodi mpya lakini Mabingwa hao wa England wamesema bado hakijasainiwa kitu.
Magazeti kadhaa huko England Leo yaliandika kuwa Rooney amesaini Mkataba mpya wa Miaka Minne na Nusu na atakuwa akilipwa £300,000 kwa Wiki na Man United.
Hata hivyo Man United imekanusha habari hizo ambazo zimedai Mkataba huo thamani yake ni Pauni Milioni 70 hadi kufikia Mwaka 2018.
Lakini imeripotiwa kuwa Msemaji wa Man United akikanusha kwa tamko: “Hamna Dili na ndio maana hatujatangaza!”
Inaaminika hadi sasa Mazungumzo kati ya pande mbili yanaendelea vizuri na wakati wowote ule makubaliano yatafikiwa.
Tangu mwishoni mwa Msimu uliopita Rooney amekuwa akihusishwa na kuihama Man United pale Meneja Mstaafu, Sir Alex Ferguson, aliposema Rooney ameomba Uhamisho kitu ambacho Rooney mwenyewe alikikanusha.
Mwanzoni mwa Msimu huu, mara mbili Jose Mourinho na Chelsea yake walitoa Ofa mbili za kumnunua Rooney lakini zote zilikataliwa na Man United ambao walisisitiza Mchezaji huyo hauzwi kwa Bei yeyote ile.
Kufuatia kuthibitika kwa kuondoka Nahodha wa Man United, Nemanja Vidic, mwishoni mwa Msimu huu na pia kutojulikana kwa hatima ya Naibu Nahodha Patrice Evra ambae Mkataba wake unamalizika mwishoni mwa Msimu huu, inatarajiwa Wayne Rooney ndie atapewa Utepe wa Nahodha wa Mabingwa hao wa England.
Mkataba wa Sasa wa Rooney na Man United unamalizika mwishoni mwa Msimu ujao.
Powered by Blogger.