Header Ads

NAIBU MEYA WA JIJI LA ARUSHA ADAIWA KUTAFUNA ZAIDI YA SHILINGI MILION 8 ZA MRADI WA KISIMA.



Naibu Meya wa jiji la Arusha Bw Prosper Msuya  ambaye pia ni diwani wa kata ya Daraja mbili Unga ltd anadaiwa kutafuna fedha zilizotolewa na manispaa kwa ajili ya kuchimba kisima cha maji katika mtaa wa Senare kiasi cha zaidi ya shl millioni 8.
Akitoa malalamiko hayo mbele ya waandishi wa habari  mjumbe wa serikali ya mtaa wa Senare Bw Aliamin Msuya amesema kuwa naibu huyo anadaiwa kutumia fedha hizo kwa matumizi tofauti kinyume na malengo ya fedha hizo kama ilivyotolewa na Almashauri.
Amesema kuwa Naibu huyo fedha hizo ziliombwa kutoka Almashauri kiasi cha shl million 16 lakini walipewa kiasi hicho cha shl 8 ambacho Msofe alikichukua na kuzitumia kwa matumizi ambayo siyo sahihi na badala yake aliwapelekea wananchi maji ambayo ni yamsaada kutoka sehemu ninyinge huku akiwalagai wananchi kuwa ilikuwa ni moja ya ahadi zake.
Bw Msuya amesema kuwa matumizi hayo yasiyo sahihi ni ubadhilifu wa fedha za serikali kwani katika matumizi ya fedha hizo hakuna kiongozi yeyote wa mtaa aliyeshirikishwa katika kikao chochote cha kujadili matumizi ya feha hizo  jambo ambalo linaashiria ubadhilifu na fedha za serikali.
Pamoja na hayo amesema katika kikao cha ODC kilichokaa kilisababisha sinto fahamu baada ya wajumbe kuhitaji kujua juu wa kuwepo kwa fedha hizo  lakini haikupatikana muafaka juu ya matumizi halisi ya matumizi ya fedha hizo.
V iongozi huo wanahoji fedha hizo zilitumika kwa kazi gani na nikwanini kazi iliyofanyia hazibaishwi kama siyo ubadhilifu hivyo kuomba kiongozi huyo kujitokeza hadharani kudhibisha matumizi halisi ya fedha hizo na wananchi wapate kuelewa.
Hata hivyo Naibu Meya huyo bw msofe hakuweza kupatikana kupitia smu yake ya mkononi ili kuweza kudhibitisha tuhuma hizi lakini bado tunaendelea kumtauta
Powered by Blogger.