Header Ads

BASATA YABARIKI TAMASHA LA PASAKA.

BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA)  mwishoni mwa wiki iliyopita lilikabidhi kibali kupitia Katibu Mtendaji wa baraza hilo, Godfrey Mngereza kwa ajili ya uendeshaji wa Tamasha la Pasaka linaloandaliwa na  Kampuni ya Msama Promotions  ya jijini Dar es Salaam. 
Tamasha hilo ni muendelezo wa Tamasha la Pasaka lililoasisiwa tangu mwaka 2000 likiwa na lengo la kumtukuza na kumtumikia Mungu kupitia nyimbo mbalimbali za waimbaji wa Tanzania na nje ya nchi.
Akizungumzia juu ya kupata kibali hicho,Mratibu wa tamasha hilo ambaye  pia ni mjumbe wa BASATA,Bwan Alex Msama,  alisema kuwa kibali kilitolewa wiki iliyopita kwa ajili ya tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika Aprili 20, jijini Dar es Salaam kabla ya kuhamia katika mikoa nane itakayochaguliwa kufanyika kwa tamasha hilo kupitia mfumo wa upigaji kura kupitia ujumbe mfupi wa maandishi.
Msama alisema taratibu za maandalizi ya tamasha hilo zinaendelea ikiwa ni pamoja na waimbaji kupigiwa kura na kufanya mazungumzo na wale watakaoshinda kwa kupigiwa kura nyingi ndio watakaotumbuiza na pia kupata mahali litakapofanyika.
“Maandalizi kwa ujumla yanaendelea vizuri kabisa, kibali kimepatikana kinachoendelea sasa ni kwamba tumewapa nafasi watanzania wenyewe wachague mgeni rasmi na waimbaji wataoimba katika tamasha la mwaka huu, kwa mgeni rasmi tunaomba waendelee kupiga kura kwa wingi ili kuchagua mahitaji hayo,” alisema Msama.
Msama amendelea kuwakumbusha watanzania namna ya kuwapigia kura waimbaji, mgeni rasmi na mikoa ambako ukitaka kumpigia mwimbaji andika pasaka acha nafsi kisha andika jina la mwimbaji unatuma kwenda namba 15327.

Pia kwa mgeni rasmi  andika neno pasaka acha nafasi kisha andika jina la mgeni rasmi unayetaka kumpigia kura tuma kwenda 15327, wakati mikoa unaandika pasaka acha nafasi jina la mkoa unaotaka kuupigia kura tuma kwenda namba 15327 piga kura uwezavyo ili upate mwimbaji na mgeni rasmi na mkoa unaopenda tamasha lifanyike.
Powered by Blogger.