Header Ads

KIMATAIFA KIRAFIKI: DIEGO COSTA KUICHEZEA SPAIN KWA MARA YA KWANZA!

>BRAZIL WAKO BONDENI!

DIEGO_COSTAJUMATANO Usiku Mechi za Kimataifa za Kirafiki zitarindima Viwanja mbalimbali Duniani na huko Madrid, Mabingwa wa Dunia, Spain, watatinga Uwanjani kujipima na Italy huku macho ya wengi yakimkodolea Straika wa Atletico Madrid, Diego Costa, akichezea Mechi ya kwanza Nchi yake mpya Spain.
Diego Costa ni Mzaliwa wa Brazil na ameshaichezea Nchi hiyo Mechi mbili za Kirafiki lakini Mwaka Jana aliamua kuikana na kuamua kuiwakilisha Spain.
Jumatano Spain watashuka Uwanja wa Vicente Calderon kucheza na Italy.
Akimuongelea Diego Costa, ambae anazo Goli 21 kwenye La Liga akiwa na Timu yake Atletico Madrid, Kocha wa Spain Vicente Del Bosque, amesema: “Yeye ni ishu ya kustaajabisha, hajaitwa Timu ya Taifa kwa sababu kazaliwa Brazil. Lakini tumemwita kwa sababu ya mafanikio yake na Klabu yake na tunaamini atatusaidia. Ndio sababu tumemwita na hatuna sababu nyingine.”
Huku akaitarajiwa kutangaza Kikosi chake kitakachokwenda kwenye Kombe la Dunia huko Brazil hapo Mei 25, Vicente Del Bosque anatarajiwa kuwapima Wachezaji kadhaa.
Nao Italy, ambao wametoka Sare Mechi zao mbili zilizopita za kujipima dhidi ya Germany na Nigeria, baada ya Mechi hii na Spain, watacheza Mechi nyingine mbili na Republic of Ireland na Luxembourg kabla ya Fainali za Kombe la Dunia ambako watafungua dimba na England huko Manaus, Brazil Juni 14.
Kwenye Mechi hii na Spain, Italy itawakosa Danielle De Rossi, Kiungo wa AS Roma ambae ameachwa baada kumtandika ngumi Mauro Icardi walipotoka 0-0 na Inter Milan Jumamosi iliyopita na pia Mario Balotelli ambae ameumia Bega.
Spain wanatinga kwenye Mechi hii wakitoka kuifunga Equitorial Guinea 2-1 na kupigwa 1-0 na South Africa Mwezi Novemba.
SOUTH AFRICA v BRAZIL
Kikosi cha Brazil, chini ya Kocha Luiz Felipe Scolari, kipo Nchini South Africa kupambana na Timu ya Taifa ya Nchi hiyo, Bafana Bafana.
Brazil wanatinga kwenye Mchi hii wakiwa wameshinda Mechi zao 6 za Kirafiki zilizopita na watacheza Mechi nyingine 3 kabla ya Fainali za Kombe la Dunia.
South Africa itaingia kwenye Mechi hii ikiwa na morali kubwa baada ya kuwatungua Mabingwa wa Dunia, Spain, Bao 1-0 Mwezi Novemba kwenye Mechi iliyochezwa Soccer City, Johannesburg.
Brazil watafungua Fainali za Kombe la Dunia hapo Juni 12 kwa kucheza na Croatia.
MECHI za KIMATAIFA KIRAFIKI
RATIBA
[Muda ukitajwa ni Bongo Taimu]
Jumatano Machi 5
Pakistan Vs Afghanistan
Honduras Vs Venezuela
Malawi Vs Zimbabwe
Morocco Vs Gabon
Mozambique Vs Angola
Senegal Vs Mali
Panama Vs Peru
Namibia Vs Tanzania
Mauritania Vs Niger
Zambia Vs Uganda
Congo Vs Libya
Grenada Vs Jamaica
12:00 Australia Vs Ecuador
13:40 Japan Vs New Zealand
15:30 India Vs Bangladesh
16:30 Burundi Vs Rwanda
20:00 Russia Vs Armenia
20:00 Georgia Vs Liechtenstein
20:00 Iran Vs Guinea
21:00 Lithuania Vs Kazakstan
21:00 Azerbaijan Vs Philippines
20:00 Hungary Vs Finland
20:00 Greece Vs South Korea
20:00 Albania Vs Malta
20:00 Algeria Vs Slovenia
20:00 South Africa Vs Brazil
20:00 Montenegro Vs Ghana
20:30 Israel Vs Slovakia
20:30 Bosnia Vs Egypt
20:30 Czech Republic Vs Norway
21:00 Cyprus Vs Northern Ireland
21:00 Macedonia Vs Latvia
21:00 Andorra Vs Moldova
21:00 Colombia Vs Tunisia
21:30 Luxembourg Vs Cape Verde
21:30 Turkey Vs Sweden
22:00 Romania Vs Argentina
22:00 Ukraine Vs United States
22:00 Gibraltar Vs Estonia
22:30 Austria Vs Uruguay
22:30 Switzerland Vs Croatia
22:45 Poland Vs Scotland
22:45 Germany Vs Chile
22:45 Belgium Vs Ivory Coast
22:45 Wales  Vs Iceland
22:45 Ireland Vs Serbia
23:00 France Vs Netherlands
23:00 England Vs Denmark
22:45 Portugal Vs Cameroon
23:00 Spain Vs Italy
23:59 Saint Lucia Vs Jamaica
Alhamisi Machi 6
1:30   Mexico Vs Nigeria
2:00   Costa Rica Vs Paraguay
Powered by Blogger.